TANGAZO


Friday, January 25, 2013

Mfanyabiashara na mkewe, waiandalia sherehe timu ya Taifa ya Kikapu ya Somalia

Balozi wa Somalia nchini Tanzania, Diriye Mohammed (kulia), akiwa na mwenyeji wake, mke wa mfanyabiashara aliyeiandalia sherehe ya kuipongeza timu ya Taifa ya nchi hiyo, iliyokuwa inashiriki katika mashindano ya mpira wa kikapu Kanda ya Tano jijini Dar es Salaam, Bi. Khadija Camalow, nyumbani kwao Mikocheni wakati wa sherehe hiyo.
Bi. Khadija Camalow, akiwa na mtoto wake, Hussein Ahmed, nyumbani kwao Mikocheni wakati wa sherehe hiyo.
Bi. Khadija Camalow, akiwa na rafiki yake Falastin, wakati wa sherehe hiyo, nyumbani kwao Mikocheni jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wachezaji wa timu ya Taifa ya mpira wa kikapu ya Somalia wakiwa katika sherehe ya kupongezwa na mfanyabiashara Ahmed Hussein Malabow na mkewe, Khadija Camalow, nyumbani kwao, Mikocheni, jijini Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo. Timu hiyo, ipo jijini Dar es Salaam, ikishiriki katika mashindao ya mchezo huo, Kanda ya Tano. (Picha zote na Kassim Mbarouk)
Kapteni wa timu hiyo, akizungumza moja kwa moja na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, wakati wa shafla hiyo, ya kupongezwa na mfanyabiashara Ahmed Hussein Malabow na mkewe, Khadija Camalow, nyumbani kwao, Mikocheni, Dar es Salaam, usiku wa kuamkia leo, huku kapeteni huyo pamoja na wachezaji wenzake wakimhakikishia Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Abdi Saaeid Shirdoon, ushindi katika michezo yao inayofuata na hatimaye kunyakua kombe la michuano hiyo. Timu hiyo, ipo jijini Dar es Salaam, ikishiriki katika mashindao ya Kanda ya Tano ya mchezo huo. 
Baadhi ya wachezaji hao, wakipata chakula cha usiku katika hafla hiyo ya kupongezwa.
Wachezaji wakila chakula walichoandaliwa na wenyeji wao, usiku wa kuamkia leo, ikiwa ni katika kupongezwa kutokana na kufanya vizuri katika michezo yao, waliyokwisha kucheza.
Bi. Khadija, akiwa pamoja na wachezaji hao wa timu ya Taifa ya Somalia, wakati wakipata mlo wa usiku katika hafla hiyo. 
Mmoja wa wachezaji hao, akizungumza moja kwa moja na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, nyumbani kwao Somalia, wakati wa hafla hiyo, wakimhakikishia ushindi na kulinyakua kombe la mashindano hayo.
Mfanyabiashara Ahmed Hussein Malabow na mkewe, Khadija Camalow, wakizungumza kwa simu moja kwa moja na Waziri Mkuu wa nchi ya Somalia, Abdi Saaeid Shirdoon na kumuahidi kuisaidia timu hiyo, hadi ifanikiwe kutimiza ahadi yake ya kunyakua ubingwa wa Kanda ya Tano ya mchezo huo. Wachezaji wengi wa Somalia wanacheza nje ya nchi katika timu mbalimbali za Ulaya na Marekani.
Bi. Khadija Camalow na mumewe, mfanyabiashara Ahmed Hussein Malabow,  wakizungumza kwa simu moja kwa moja na Waziri Mkuu wa nchi ya Somalia, Abdi Saaeid Shirdoon na kumuahidi kuisaidia timu hiyo, hadi ifanikiwe kutimiza ahadi yake ya kunyakua ubingwa wa Kanda ya Tano ya mchezo huo. Wachezaji wengi wa Somalia wanacheza nje ya nchi katika timu mbalimbali za Ulaya na Marekani.
Balozi wa Somalia nchini Tanzania akizungumza moja kwa moja na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Abdi Saaeid Shirdoon katika hafla hiyo, akimuahidi ushindi katika michezo itakayocheza timu hiyo, hadi kunyakua ubingwa wa mashindano hayo.
Baadhi ya wachezaji hao wa timu ya Taifa ya Somalia, wakiwa tayari kukata keki waliyoandaliwa, kwenye hafla hiyo na wenyeji wao. 
Wachezaji wa timu ya Taifa ya Somalia, wakikata keki waliyoandaliwa, kwenye hafla hiyo na wenyeji wao, Mfanyabiashara Ahmed Hussein Malabow na mkewe, Khadija Camalow.
Mtoto Iman, naye akikata keki ya kuadhimisha kuzaliwa kwake katika hafla hiyo.
Kapteni wa timu hiyo, akimpongeza mtoto Iman, kwa kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwake katika hafla hiyo.
Mfanyabiashara Ahmed Hussein Malabow, akimlisha keki mtoto wa mdogo wake, Iman wakati akiadhimisha siku ya kuzaliwa kwake katika hafla hiyo. Kushoto ni baba wa Iman.
Balozi wa Somalia nchini Tanzania, Mohamed Duriye,  akizungumza katika hafla hiyo.


Wachezaji wa timu hiyo, wakipiga picha ya pamoja na wenyeji wao, mwisho wa hafla hiyo.

No comments:

Post a Comment