TANGAZO


Sunday, January 13, 2013

Azam yaendelea kulebeba Kombe la Mapinduzi, Makamu wa Pili Zanzibar, Balozi Idd awakabidhi Kombe

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd, akiikagua timu ya Azam FC, wakati timu hiyo, ilipopambana na Tusker FC ya Kenya katika Fainali za Kombe la Mapinduzi, Uwanja wa Aman, mjini Zanzibar usiku wa kuamkia leo. (Picha zote na Martin Kabemba)

Kikosi cha Azam FC, wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya mchezo wa Fainali na Tusker FC ya Kenya, usiku wa kuamkia leo, Uwanja wa Aman, mjini Zanzibar. 
Mchezaji Himid Mao wa Azam FC, akiudhibiti mpira mbele ya wachezaji wa Tusker FC ya Kenya wakati wa mchezo huo wa fainali wa Kombe la Mapinduzi dhidi ya Tusker ya Kenya. Azam FC, ilishinda mabao 2 - 1 na kukabidhiwa Kombe na sh. milioni 10 taslimu. 
Katika mchezo huo kulitokea kituko baada ya msichana ambaye jina lake halikujulikana kuingia  uwanjani wakati pambano likiendelea na kusababisha mchezo kusimama kwa muda. Pichani Refarii wa mchezo huo, Shibo akimtoa msichana huyo uwanjani.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd akikabidhi kombe kwa Nahodha wa timu ya Azam FC. Himid Mao Mkami baada ya mchezo wa fainali kwa kuilaza Tusker ya Kenya 2 - 1.

No comments:

Post a Comment