Naibu Waziri wa Fedha, Saada Salum akizungumza na wahitimu 1,331 wa Chuo cha Uhasibu, Singida (TIA), kwenye mahafali ya 10, jana. (Picha na Hillary Shoo)
| Na Hillary Shoo, SINGIDA.
WAHITIMU wa kozi mbalimbali
katika chuo cha uhasibu tawi la Singida (TIA), wametakiwa kuweka
uadilifu mbele popote watakapokuwa kwa kuwa ndiyo dira sahihi ya maisha
yao.
Hayo yamebainishwa
jana mjini hapa na Naibu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya Salum, wakati wa sherehe
za mahafali ya kwanza ya Tawi hilo zilizofanyika Chuoni hapo eneo
la Ginnery mjini Singida.Naibu Waziri huyo
alisema kuwa taaluma ya uhasibu ni taaluma iliyotukuka hivyo ni jambo zuri
iwapo watu walioisomea watazingatia miiko na kanuni zake kwa kiwango cha hali ya
juu.Alieleza kuwa kashfa
mbalimbali zinazosikika nchini na kwingineko duniani ni matokeo ya watu kukosa
uadilifu na hivyo kujiingiza katika vitendo viovu.“Naomba kuwakumbusha
kwamba mtakapotoka hapa baada ya kuhitimu masomo yenu, mtakutana na changamoto
mbalimbali, ila mkumbuke tu kwamba ni uadilifu pekee ndio utakaowaongoza katika
maisha yenu yote” alifafanua.
Aliwataka wahitimu hao kutumia vema elimu waliyoipata
katika kubuni, kuanzisha na kusimamia shughuli mbali mbali ya kibiashara
zitakazowasaidia wao na jamii yote ya Watanzania kwa kuleta
maendeleo.
“Enzi ya kutaraji kuajiriwa na serikali imepitwa na
wakati. Wekeni mawazo yenu sasa katika kujiajiri wenyewe kwani elimu mliyopata
inatosha kuwawezesha kupambana vizuri na changamoto zozote
mtakazokumbana nazo. “ Alisema.
Aidha, Salum alitoa mwito kwa wahitimu hao kutotosheka na
elimu waliyopata bali wajiendeleze zaidi na kuhakikisha wanafikia malengo
wanayojiwekea.Awali, Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TIA,
Shah Hanzuruni alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa Tawi la TIA
Singida linakabiliwa na uhaba mkubwa wa madarasa, nyumba za wahadhiri, kumbi za
mihadhara, samani, maktaba ya kisasa na wahadhiri.Jumla ya wahitimu
1,331, wakiwemo wanawake 662 na wanaume 669, walitunukiwa vyeti na stashahada za
fani mbalimbali ikiwemo uhasibu, uboharia, raslimali watu na biashara.
|


No comments:
Post a Comment