TANGAZO


Monday, December 10, 2012

Miyeyusho amaliza kazi kwa Nassibu katika raundi ya 10 PTA, Waziri Mukangala ashuhudia kichapo

 
Bondia Francis Miyeyusho akiwa amebebwa na mashabiki wake kwenye ukumbi wa PTA, Saba Saba, Temeke jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo baada ya kutetea mataji yake ya  Kimataifa kwa kumpiga Nassib Ramadhan kwa Technical Knockout (TKO) ya raundi ya 10.

Kwa Hisani ya Bin Zubeiry Blog
BONDIA Francis Miyeyusho ‘Chichi Mawe’ amefanikiwa kutetea taji lake la WBF uzito wa Bantam, baada ya kumpiga Nassib Ramadhan kwa Techinical Knockout (TKO) ya raundi ya 10 kwenye ukumbi wa PTA, Saba Saba, Temeke mjini Dar es Salaam usiku huu huku akishuhudiwa na Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk, Fenella Mukangala.
 
Nassib alionekana kuishiwa pumzi tangu raundi ya nane, lakini alijikongoja kutaka kumaliza raundi 12 za pambano hilo, ila kwa bahati mbaya, safari ikaishia raundi ya 10.
 
Hata hivyo, Nassib bondia kutoka Mabibo, jijini Dar es Salaam, alilianza vizuri pambano hilo akimsukumia mpinzani wake makonde mazito yaliyoonekana kumyumbisha.
 
Naasib aliendelea kutawala pambano hilo hadi raundi ya sita, baada ya hapo, mwelekeo wa pambano ulianza kubadilika taratibu, Chichi, mtoto wa Kinondoni akianza kumuadhibu mpinzani wake kwa makonde yake yaliyoshiba uzito.
 
Nassib alijitahidi mara moja moja kujibu mapigo, lakini zaidi alitumia ujanja wa kumkumbatia Chichi ili kumpunguza kasi.
 
Hata hivyo, Nassib hakushindwa kwa kupigwa ngumi, bali aliishiwa pumzi jambo ambalo linaashiria kijana huyo ni bondia imara na anaweza kuwa mpinzani wa kweli wa Chichi Mawe.
 
Kwa ujumla lilikuwa pambano zuri ambalo kwa muda mrefu halijapatikana katika ardhi ya Tanzania- mabondia walikuwa wakipigana, hakukuwa na ujanja ujanja. Wote ni mafundi na mamia waliohudhuria pambano hilo, waliburudika kwa mchezo mzuri.
 
Katika mapambano ya awali, Deo Samuel alitoka sare na Freddy Sayuni, Mohamed Matumla alimpiga kwa Knockout (KO) raundi ya pili Deo Miyeyusho, Fadhil Majiha alimpiga kwa pointi Juma Fundi na Ibrahim Classic alimpiga kwa pointi Said Mbugi.
 
Mgeni rasmi, Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangara alimvalisha mkanda wa ubingwa Miyeyusho baada ya pambano hilo, lililohudhuriwa pia na Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’. 
 
Mbwana Matumla katikati akiwa na George Njavike (kulia) na kushoto, King Kiboya. 

Hassan  Matumla kiwa na mkewe wakifuatilia pambano hilo.

Promota Mohamed Bawaziri akiteta jambo na Waziri Dk. Fenella

Jamaa alizima mapemaaa, hajaangalia pambano sasa sijui atasimulia nini kitaa

Ibrahim Classic (kushoto) akimuadhibu Said Mbugi

Bondia mstaafu, Koba Kimanga (kulia), akizungumza jambo na Thomas Mashali

Msafiri Mgoyi (kushoto) wa TFF, akizungumza jamba na Yassin Ustadh

Mabondia wastaafu, Emmanuel Mlundwa (kulia) na Habib Kinyogoli, wakizungumza jambo kwenye mpambano huo.

Mohamed Matumla (kushoto), akimuadhibu Deo Miyeyusho

Mohamed Matumla (kushoto), akiendelea kumuadhibu Deo Miyeyusho

Mohamed Matumla akiwa amebebwa juu baada ya kushinda pambano lake na Deo Miyeyusho kwa KO raundi ya pili.

Juma Fundi (kulia), akimtupia konde Fadhil Majiha

Jaji akifuatilia kwa makini pambano

Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto (kulia), akifurahia jambo na Waziri Dk. Fenella Mukangala katika meza kuu.

Kutoka kulia, ni Makamu Mwenyekiti wa Simba SC, Geoffrey Nyange 'Kaburu', Mzee Matumla na Benny Kisaka.

Bondia Nassib akimtupia konde Francis Miyeyusho

Nassib na Miyeyusho wakipambana

Nassib akimpiga ngumi Miyeyusho

Nassib na Miyeyusho wakitafutana

Miyeyusho akimchimbua Nassib ngumi ya kidevu katika mpambano wao huo.

Nassib na Miyeyusho wakitupiana ngumi

Konde la Miyeyusho limetua kwenye uso wa Nassib

Nassib na Miyeyusho wakisukumiana ngumi

Nassib na Miyeyusho wakipambana kwa kila mbinu

Nassib na Miyeyusho wakisukumiana makonde

Nassib akimtupia konde Miyeyusho (kulia) naye Miyeyusho kama anamwambia nimeiona hiyo.

Hapa ikawa tena piga nikupige kati ya mabondia hao, Nassib na Miyeyusho

King Miyeysho ukipenda muite Chichi Mawe, akinyanyuliwa juu na mashabiki wake baada ya kumtwanga kwa TKO, Nassib katika raundi ya 10.

Nassib akiwa amebebwa kutolewa ulingoni baada ya kula kichapo kutoka kwa Miyeyusho cha TKO katika raundi hiyo.

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukangala, akimvalisha mkanda Miyeyusho. Kushoto ni promota wa pambano hilo, Mohamed Bawaziri.

No comments:

Post a Comment