TANGAZO


Tuesday, October 16, 2012

Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa aongoza Harambe ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kiislamu ya Lambo mjini Mwanga, mkoani Kilimanjaro



Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na baadhi ya viongozi wa dini ya kiislam wa Wilaya wa Mwanga mkoani Kilimanjaro,wakati alipokuwa akiwasili kwenye hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa shule ya sekondari ya kiislam ya Lambo huko Mwanga mkoani Kilimanjaro iliyofanyika mwishoni mwa wiki.Kushoto ni Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe.

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mhe. Edward Lowassa akizungumza waumizi wa dini ya kiislam waliohudhulia hafla ya harambee ya kuchangisha fedha za ujenzi wa shule ya sekondari ya kiislam ya Lambo huko Mwanga mkoani Kilimanjaro, iliyofanyika mwishoni mwa wiki. Mhe. Lowassa alichangia sh. millioni 10 na kusema Bakwata wilayani Mwanga ni mfano wa kuigwa kwa kuwekeza katika elimu. Kulia ni Waziri wa Maji, Prof. Jumanne Maghembe.

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa akiendelea kuchangisha kwenye harambee hiyo.

Waziri Mkuu wa zamani na Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mhe. Edward Lowassa akipongezwa na baadhi ya Masheikh wa Wilaya ya Mwanga,Mkoani Kilimanjaro mara baada ya kuongoza harambee hiyo ya kuchangisha fedha za ujenzi wa shule ya sekondari ya kiislam ya Lambo huko Mwanga mkoani Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment