
"Mahakama ya rufaa inaona kuwa katika hali hii, uamuzi wowote katika mahakama ya kabla ya kesi, kuhusu Bwana Gbagbo kuendelea na kifungo au kuachiliwa kwa sababu ya afya yake, utakuwa umechukuliwa mapema mno.
Kwa hivo mahakama ya rufaa inaona kuwa mahakama yaliyotangulia kesi hayakukosa kwa kutozingatia afya ya Bwana Gbagbo katika hali ya sasa."
Bwana Gbagbo anakabili mashtaka ya uhalifu dhidi ya binaadamu wakati wa ghasia zilizofuatia uchaguzi miaka miwili iliyopita.
Watu zaidi ya 3000 waliuwawa na malaki walihama makwao, baada ya Bwana Gbagbo kukataa kwamba alishindwa kwenye uchaguzi.

No comments:
Post a Comment