TANGAZO


Thursday, August 9, 2012

Rais Kikwete awaapisha Watendaji Wakuu wa Mahakama


 Rais Dk.Jakaya Mrisho Kikwete leo, amewaapisha Mtendaji Mkuu wa Mahakama pamoja na Msajili Mkuu wa Mahakama na Msajili wa Mahakama ya Rufani katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam. Walioapishwa ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama Hussein Katanga, Msajili Mkuu wa Mahakama, Ignus Paul Kitusi na Msajili wa Mahakama ya Rufani, Panterine Muliisa Kente. Pichani Mtendaji Mkuu wa Mahakama, Hussein Katanga akiapa mbele ya Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu jijini Dar es Salaam. 

Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, akiwa katika picha ya pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue (kushoto) pamoja na Maofa Waandamizi wa Mahakama, aliowaapisha leo asubuhi, Ikulu jijini Dar es Salaam. Wapili kushoto ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama  Hussein Katanga, wanne kushoto) ni Msajili Mkuu wa Mahakama, Ignus Paul Kitusi na kulia ni Msajili wa Mahakama ya Rufani, Panterine Muliisa Kente. (Picha zote na Freddy Maro)

No comments:

Post a Comment