Waziri Mkuu Mizengo Pinda akifungua mafunzo ya wakufunzi wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 kwa ngazi ya kitaifa mjini Dodoma. Sensa hiyo inatrajia kufanyika nchini kote tarehe 26 mwezi Agosti mwaka huu. Akifungua mafunzo hayo Waziri Mkuu huyo amewaomba wabunge, viongozi wa dini na vyama vya kisiasa, watendaji wa kati, wenyeviti wa mitaa na vijiji , masheha na wadau kushirikiana katika kuelimisha na kuhamasisha jamii ili iweze kushiriki kikamilifu katika sensa. (Picha zote na Tiganya Vincent- MAELEZO).
Waziri Mkuu Mizengo Pinda (katikati) akibadilishana mawazo na Waziri wa Fedha Dk William Mgimwa (kulia) na Kamishna wa Sensa Hajjat Amina Mrisho mara baada ya kufungua mafunzo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 kwa ngazi ya kitaifa mjini Dodoma.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa pili kushoto) akibadilishana mawazo na Waziri wa Fedha Dk William Mgimwa (wa pili kulia) na Kamishna wa Sensa Hajjat Amina Mrisho (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dk. Servacius Likwelile mara baada ya kufungua mafunzo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 kwa ngazi ya kitaifa.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wakufunzi wa sensa ya watu na makazi kwa ngazi ya kitaifa mara baada ya kufungua mafunzo ya sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 kwa ngazi ya kitaifa mjini Dodoma. Sensa hiyo inatrajia kufanyika nchini kote tarehe 26 mwezi Agosti mwaka huu.

No comments:
Post a Comment