TANGAZO


Thursday, May 24, 2012

Naibu Waziri Makamba atembelea TCRA



Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba akipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Profesa John Nkoma (kushoto), wakati alipotembelea Makao Makuu ya Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania zilizopo jengo la Mawasiliano Tower, Barabara ya Sam Najoma jijini Dar es Salaam leo, kujionea shughuli zinazofanywa na Mamlaka hiyo.

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (wa pili kushoto), akimsikiliza Mhandisi Mfawidhi wa Mawasiliano ya Redio wa Mamlaka ya Mawasilioano Tanzania, Johannes Magesa, wakati alipokuwa akitoa maelezo juu ya kutambua muingiliano wa mawasiliano kwa masafa ya redio. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Profesa John Nkoma.

Naibu Waziri Makamba (kulia) akimsikiliza Mhandisi wa TCRA, Ikuja Jumanne wakati  aliokuwa akioneshwa kifaa cha kupimia masafaa ya Radio na Televisheni, alipotembelea Mamlaka hiyo.

Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (katikati), Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Profesa John Nkoma, wakioneshwa kifaa kinachotumika kupimia mionzi ya minara mbalimbali hapa nchini na Meneja wa Mipango na Utafiti wa TCRA, Dk. Ali Simba.

Ofisa Habari wa TCRA, Doris akiwa na wafanyakazi wenzake wakifuatilia kwa makini hotuba ya Naibu Waziri Makamba, alipokuwa akiongea na wafanyakazi wa Mamlaka hiyo jijini leo.

No comments:

Post a Comment