TANGAZO


Sunday, March 4, 2012

Mahafali ya Wahitimu wa Shahada ya Uzamili ya Usimamizi Biashara ya Kimataifa

Mhitimu Mathew Shayo, akipokea cheti cha kuhitimu Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Biashara za Kimataifa, kutoka Chuo Kikuu cha Biashara za Kimataifa cha India (IIFT), kutoka kwa Mkurugenzi wa Chuo hicho, Thomas Chako, Dar es Salaam jana. IIFT huendesha kozi hiyo ya MBA-IB kwa ushirikiano na Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM), Dar es Salaam. Wanaoshuhudia ni Makamu Wakuu wa Chuo cha IFM, Profesa Isaya Jairo (wa pili kulia) na Profesa Tadeo Satta.

Mkurugenzi wa Chuo cha Biashara za Nje, cha nchini India (IIFT), Thomas Chako akiongea katika mahafali ya 12 ya Shahada ya Uzamili, inayotolewa na Chuo hicho kwa ushirikiano na Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM ) cha Dar es salaam. Chako alikabidhi veti kwa wahitimu takribani 31. Wengine pichani, kutoka kulia ni Makamu Wakuu wa Chuo cha IFM Prof. Jairo na Prof. Tadeo Satta na Mkuu wa Chuo hicho Prof. Godwin Mjema. Chako alihimiza umuhimu wa Tanzania kuzalisha wataalamu wa kutosha wa biashara za Kimataifa ili kunufaika na fursa za biashara za ulimwengu.

No comments:

Post a Comment