TANGAZO


Sunday, December 6, 2015

Serikali yaahidi kuendelea kuweka mazingara bora na wezeshi katika Tasnia ya Filamu

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Mwamini Juma Malemi (kushoto) akiwasili kuelekea kufungua kikao cha wadau wa Filamu kujadili namna ya kuimarisha na kuboresha miundombinu katika tasnia ya filamu juzi Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo na kulia ni Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini Bw. Simon Mwakifwamba. 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Mwamini Juma Malemi (katikati) akizungumza na wasanii pamoja na wadau wa filamu (hawapo pichani) wakati wa kufungua kikao cha wadau wa Filamu kujadili namna ya kuimarisha na kuboresha miundombinu katika tasnia ya filamu juzi Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo na kulia ni Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini Bw. Simon Mwakifwamba. 
Wasanii na wadau wa filamu wakisikiliza kwa makini mada zilizokua zikiendelea wakati wa kikao cha wadau wa Filamu kujadili namna ya kuimarisha na kuboresha miundombinu katika tasnia ya filamu juzi Jijini Dar es Salaam. 
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Mwamini Juma Malemi (katikati waliokaa) katika picha ya pamoja na wasanii na wadau wa filamu nchini juzi jijini Dar es Salaam baada ya kufungua  kikao cha wadau wa Filamu kujadili namna ya kuimarisha na kuboresha miundombinu katika tasnia ya filamu. Wapili kulia ni Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo na wapili kushoto ni Rais wa Shirikisho la Filamu Nchini Bw. Simon Mwakifwamba. (Picha zote na Genofeva Matemu - Maelezo)

Na Genofeva Matemu – Maelezo
06/12/2015

Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Mwamini Juma Malemi wakati wa ufunguzi wa kikao cha wadau wa Filamu kujadili namna ya kuimarisha na kuboresha miundombinu katika tasnia ya filamu juzi Jijini Dar es Salaam.

Kama Ilani ya mwaka 2015 – 2020 ilivyodhihirisha serikali itaendelea kuimarisha uwezo wa Bodi ya Filamu nchini ili isimamie kwa ukamilifu utekelezaji wa sheria zinazohusu shughuli za filamu na ubunifu kwa lengo la kulinda haki na maslahi ya wanatasnia wa filamu” alisema Bibi Malemi.

Aidha Bibi. Malemi amewakumbusha wasanii kutekeleza  sheria, kanuni na taratibu kwani ni wajibu wa kila mtu kutii bila shuruti na kuwataka kutambua ya kuwa utekelezaji wa sheria hauna mbadala na siyo wa hiari.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji Bodi ya Filamu Bibi. Joyce Fisoo amesema kuwa  kikao kazi cha wadau filamu kinatoa fursa kwa wadau wote wa tasnia ya filamu  kujifunza kutoka kwa wataalamu mbinu mbadala za kimaendeleo pamoja na kutoa fursa ya kujitathmini wao wenyewe ili kuweza kufikia azma yao na azma ya kuinua tasnia ya filamu nchini.

Naye msanii wa filamu nchini Bibi. Coletha Raymond amesema kuwa kikao cha wadau wa filamu kimefanyika wakati muafaka na kuviombavyombo husika pamoja na wasanii kushirikiana kuunganisha nguvu kutekeleza yale watakayoyaainisha katika kikao hicho kinacholenga kuboresha tasnia ya filamu nchini.


Bibi Coletha amewataka wasanii wasiwe wabishi na kung’ang’ania kufanya kitu cha aina moja bali wawe wabunifu kwani mchango wa wasanii umekua ukionekana katika matukio mbalimbali yakitaifa na yasiyo yakitaifa.

No comments:

Post a Comment