TANGAZO


Saturday, July 25, 2015

Wizara ya Nishati na Madini yaanza mafunzo kuhusu huduma za leseni za madini kwa njia ya mtandao katika Kanda ya Kaskazini

Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Afisa Madini Mkazi – Kilimanjaro kabla  ya  kuanza kwa uendeshaji wa mafunzo ya huduma  za leseni kwa njia ya mtandao.  Mafunzo hayo yanahusisha wachimbaji wa madini lengo likiwa ni kuwapa uelewa wa matumizi ya huduma za leseni kwa njia ya mtandao. 
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe akielezea mikakati ya  Wizara katika  uboreshaji wa huduma za leseni kwa wachimbaji wa madini (hawapo pichani) katika mafunzo yaliyofanyika  wilayani Same mkoani Kilimanjaro. 
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Kitengo cha Leseni Charles Gombe akisisitiza jambo katika mafunzo hayo. 
Baadhi ya wachimbaji wa madini  kutoka wilaya ya  Same mkoani Kilimanjaro wakifuatilia kwa makini mada  zilizokuwa zinawasilishwa na wataalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini (hawapo pichani). 
Mmoja wa wachimbaji wa madini kutoka  wilayani Same, mkoani Kilimanjaro Richard Mbwambo akiuliza swali katika mafunzo hayo. 
Ofisa Madini Mkazi, Mkoa wa Kilimanjaro, Fatuma Kyando akielezea  sheria na kanuni za uchimbaji wa madini  nchini katika mafunzo hayo. 
Mmoja wa wachimbaji wadogo, Naamin Samuel kutoka kampuni ya Kivoroi na Ndarauoi akiuliza swali katika mafunzo hayo. 
Mtaalam kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Idara ya Uhasibu Erick Mkumbo akifafanua jinsi ulipaji wa leseni za madini unavyofanyika. 
Wataalam kutoka  Wizara ya Nishati na Madini ( waliokaa mbele) wakiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo  waliosimama nyuma. 
Baadhi ya watoto kutoka wilayani Same mkoani Kilimanjaro wakipozi katika picha ya pamoja mbele ya  gari la matangazo la Wizara ya Nishati na Madini lililokuwa linatumika wakati wa zoezi la uhamasishaji  wa matumizi  ya huduma za leseni  za madini kwa njia ya mtandao.

No comments:

Post a Comment