Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sabodo kidato cha nne wakitoa maelezo kwa wageni wanaotembelea maonesho ya Serikali za Mitaa (ALAT), yanayofanyika katika Uwanja wa Mashujaa mkoani Mtwara.
Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Rahaleo wakijifunza kwakutumia kompyuta masomo mbalimbali, ikiwemo Hesabu katika maonesho ya Serikali za Mitaa (ALAT).
Na mwandishi wetu
KUFATIA Mkoa wa Mtwara kuwa
wenyeji wa maonesho ya Serikali za Mitaa banda la Wilaya ya Mtwara limekuwa likivutia vijana wengi kutokana na kuweka vifaa vya elimu ambayo
vinawafanya wajifunze zaidi.
Maonesho hayo yatakayodumu
kwa siku saba sambamba na elimu mbalimbali kutolewa wanafunzi wa Shule ya Sekondari Sabodo wamepata nafasi ya kujifunza na kutoa elimu kwa tu malimbali
kuhusu umuhimu wa masomo ya Sayansi.
Wanafunzi hao ambao
wanatumia maabara inayohamishika ili kutoa hamasa kwa wanafunzi wa shule
zingine kuhamasika katika kujifunza na kuyapenda masomo yasayansi ambayo kwa
kiasi kikubwa wamekuwa wakiyaogopa.
Editha Masia mwanafunzi wa
kidato cha nne shule ya sekondari Mustapha sabodo anasema kuwa katika masomo ya
sayansi amekutana na changamoto nyingi ambazo zimeweza kumsaidia kujifunza
zaidi.
Anasema kuwa uwepo wa masomo
hayo unatoa nafasi kwa wanafunzi kujifunza ili waweze kuwa wataalam wa baadae
sio kuyakimbia hali ambayo inapelekea madktari na walimu kupungua kwa kiasi
kikubwa.
“Masomo haya ni mazuri
endapo mwanafunzi atajifunza kwa vitendo unajua hiki kigololi nilichoshika bila
sayansi kinaweza kupitiliza katika hili lingi lakinikwakutumia sayansi naweza
kulikuza ikashindwa kupita hapa katika hili tundu” alisema Masia
Nae Issa Juma mwanafunzi wa
kidato cha nne shule ya sekondari Mustapha sabodo anasema kuwa wazazi wanapaswa
kuhamasisha watoto wao kujifunza masomo ya sayansi ili waweze kujifunza mengi
ambayo yanaweza kuwasaidia katika siku zijazo.
Anasema kuwa uoga wa
kuchukua masomo ya sayansi ni sababu ya wanafunzi hao kuogopa kuyasoma hivyo
kuambukizana ili hali masomo hayo yanaonyesha upendeleo hasa unapofika katika
ngazi ya elimu ya juu.
“Sayansi inatoa madaktari,
wanasayansi, walimu na kada zingine nyingi lazima tutumie njia za makusudi ili
kuweza kuhamasisha wanafunzi wengi kukimbilia masomo hayo muhimu kwa dunia ya
sasa” alisema Juma
Kwa upande wa shule za
msingi katika banda la maonyesho la mtwra mikindani hawakuwaacha wanafuzi wa
shule za misingi ambao kwa sasa wako likizo kwa kuwawekea komputa na jinsi ya
kujifunza kwa lugha za alama ambazo zinasaidia watu wenye ulemavu kuelewa
zaidi.
Wanafunzi hao walionyesha
ustadi wa kutumia komputa hizo za kujifunzia ambazo kwa kiasi kikubwa zimeweza
kuhamasisha wanafunzi kudhuria masomo kwa wakati na kupunguza utoro kwa
wanafunzi wa madarasa ya chini la kwanza na darasa la pili.
Kwa upande wa halmashauri ya
mji wa masasi wamelalamikia ukosefu wa
vipimo katika shule za watoto wenye mahitaji maalumu umepunguza idadi ya
uandikishwaji watoto wenye umri wa kwenda shule kwa lengo la kufanikisha
Mapango wa Matokea Makubwa sasa (BRN).
Nae Afisa Elimu Maalum wa Halmashuri ya Masasi
Mkoani Mtwara, Adrew Magani akitoa maelekezo kwa wananchi katika Maonyesho ya
Serikali za Mitaa (alat) katika viwanja vya Mashujaa Mjini hapa anasisitiza
wazazi wenye watoto wenye ulemavu kupeleka watoto wao shuleni na kuacha tabia
ya kuwaficha majumbani.
Hata hivyo anaongeza kuwa
endapo wazazi watapata mwamko zoezi hilo la undikishaji linaweza kufikia
malengo ya BRN kama kituo cha watoto wa mahitaji
maalum kitakuwa kinafanyakazi yake ipasavyo.
Magani anasisitiza kuwa
kutokana na hilo Halmashari hiyo baada ya kuona umuhimu wa kituo hicho cha
upimaji wakaamu kuleta kituo hicho katika Maenesho hayo ili watanzania waweze kujifunza hasa wa mkoani hapa jinsi ya
kuwasidia watoto wenye mahitaji maalum.
Aidha Afisa huyo anasema
kuwa maonyesho hayo yana umuhimu mkubwa kutokana na kuwafundisha watu
mbalimbali jinsi ya kuwasaidia watoto hao ili waliowaficha waweze kuwafichua na
kuwapeleka shuleni.
“ Maonyesho haya ni muhimu
sana… kwetu kwa sababu tunawaelekeza
jamii kuona jinsi gani tunaweza kuwahudumia watoto wenye mahitaji maalum ili
wale ambao wamewafisha waweze kuwafichua na kuwapeka shuleni ndio maana
tunawaonyesha jinsi tunavyoweza kuwahudumia.” Alisema Magani
Hata hivyo aliongeza kuwa
watoto wenye mahitaji maalum wanaweza kuchanganyika katika Darasa Moja na
watoto wengine kulingana na uelewa wao
ili kutimiza ile Lengo la Elimu Jumuishi linaweza kukamilika.
“Walemavu ni wengi lakini
hawapati nafasi ya kupata kile ambacho wengine wanakipata wakiwa shuleni ndio
maana tunahamasisha wazazi kuwatoa ndani watoto waliowafungia ili waweze kupata
haki zao za msingi……
“Hawa watoto wanapaswa kujifunza lakini wazazi wengi wanaficha hawawa peleki shuleni hivyo kukosa haki yao ya msingi ya kupata elimu hakuna mtoto ambae hawezekani wote wanafundishwa na wakaelewa kulingana na uwelewa wao na wanaweza wakachanganyika na watoto wengine katika darasa moja na ile lengo la elimu jumuishi linaweza kukamilika” alisema Magani.

No comments:
Post a Comment