| Waumini wakiwa katika kanisa la PEFA jana kwenye hitimisho la kongamano la vijana ambalo limefanyika kwa takribani siku saba. (Picha zote na Frankius Cleophace) |
Waumini wakiwa katika kanisa la PEFA jana kwenye hitimisho la kongamano la
vijana ambalo limefanyika kwa takribani siku saba.
Na Frankius Cleophace Tarime.
KANISA la Pentecostal
Evangelistc Fellowship Of Afrika lililopo Mji mdogo wa Sirari mpakani mwa nchi za Tanzania na Kenya, wilayani Tarime, mkoani Mara, wametoa mafunzo ya
Ujasiliamali kwa vijana zaidi ya miatano
kwa lengo la kuwajengea uwezo ili kuondokana na utegemezi huku wakifundishwa
uhaminifu katika maisha yao jamba ambalo litatumika kumutukuza mwenyezi mungu
na kubadili mienendo na tabia za vijana hao.
Akiongea na mwandishi wa habari hizi, Mchungaji Stive Mhechi ambaye pia alikuwa mmoja kati ya Walimu walikuwa wakitoa
mafunzo kanisani hapo alisema kuwa kanisa limeamua kukutanisha vijana hao kutoka makanisa yote ya Pefa yaliyomo ndani ya
wilaya ya Tarime kwa lengo la kuwajengea uwezo mkubwa ili waweze kuondokana na
utegemezi huku wakisudia kumutumikia mwenyezi Mungu.
Aidha Mchungaji huyo alisema
kuwa vijana hao wameweza kufundishwa mada uhaminifu katika suala la bihashara
na wale ambao wameoa wamefundishwa uhaminifu katika ndoa.
“Tumekuwa tukiona Ndoa za
watu wengi zinaharibika kwa sababu ya ukosefu wa uhaminifu hivyo kupitia
mafunzo haya itasaidia kubadili mienendo na tabia za vijana wetu ambao
tumeendelea kuwaea kiroho na kimwili” alisema Mchungaji
Mafunzo hayo yamefanyika
kanisani hapo takribani wiki moja kwa lengo la kuwajengea uwezo vijana hao ili
waweze kuondokana na utegemezi ususani vijana wanaoisha maeneo ya mipakani wamekuwa
wakitegemea ajira kutoka serikalini hivyo kupitia mafunzo hayo vijana hao
wataweza kkujishughulisha.
Kwa upande wake mwenyekiti wa
vijana Kanisa la Pefa Wilayani hapa Barnanabas Mchuma alimetumia nafasi hiyo
kuiomba serikali kuzidi kusikiliza kilio cha vijana ili waweze kuondokana na
utegemezi.
“Sisi kama kanisa tumeweza
kutoa mafunzo haya ya ujasiliamali pamja na mafunzo ya kiroho hivyo serikali
nao awewze kutuunga mkono ili kuweza kukomboa vija na kukuza uchumi wa
Taifa”alisema Mchuma.

No comments:
Post a Comment