TANGAZO


Tuesday, June 16, 2015

Mwenge wa Uhuru waingia Wilaya ya Mvomero

*Kiongozi wa mbio za Mwenge awataka wananchi kujiandikisha Daftari la Wapiga Kura

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rajab Rutengwe akiwa ameshika mwenge wa Uhuru baada ya kupokea kwa Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Said Magalula. (Picha zote na Andrew Chimesela, Morogoro)
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Rajab Rutengwe (kushoto) akiwa amekumbatiana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Mhe. Said Magalula baada ya kukabidhiwa Mwenge wa Uhuru. 
Kiongozi wa mbio za Mwenge Kitaifa Bw. Juma Khatib (katikati) akipewa maelezo ya  zoezi la uandikishaji wa wapiga kura litakavyoendeshwa, muda mfupi baada ya kuzindua zoezi hilo. (Kulia mwenye tracksuit) ni Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Betty Mkwasa. 
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru kitaifa Bw. Juma Khatibu  Chum akifungua kitambaa kama ishara ya kuzindua zoezi la uandikishaji wapiga kura Wilayani Mvomero lililofanyika  katika Kijiji cha Salawe Kata ya Kibati.

Na Andrew Chimesela (Morogoro)
0719 11 22 99/0785 336 335
(15 Juni, 2015)
Kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru Kitaifa Ndugu juma Khatibu Chum amewataka wananchi wa Mkoa wa Morogoro kujiandikisha kwenye daftari la wapiga kura ili kutumia haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi kwenye uchaguzi Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Juma Kghatibu ameyasema hayo leo wakati akitoa ujumbe wa Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa mkesha wa mwenge eneo la Kichangani katika Tarafa ya Tuliani Wilayani MvomeroMkoani Morogoro.

Amesema mwananchi yeyote ambaye amefikisha umri wa mika 18 na mwenye sifa zote za kuandikishwa  aende kujiandikisha ili aweze kupata fursa ya kuchagua viongozi bora watakaoiongozi nchi katika Serikali ya awamu ya tano.

“Hakuna nchi yeyote duniani yenye maendeleo bila ya viongozi bora. Na huwezi kupata viongozi bora nje ya uchaguzi Mkuu. Ni lazima tujiandikisha na kuchagua viongozi bora itakapofika mwezi Oktoba, uchaguzi ni haki yetu ya kidemokrasia, na ni haki yetu ya Kikatiba”. alisema Bwana Khatibu.

Mapema akiwa Wilayani Mvomero ikiwa ni Wilaya ya kwanza kukimbiza mwenge wa Uhuru katika Mkoa wa Morogoro, Kiongozi huyo wa mbio za Mwenge Kitaifa alizindua zoezi la uandikishaji wapiga kura kwa kutumia mfumo wa BVR katika kijiji cha Salawe kilichoko Kata ya Kibati Wilayani humo tayari kwa  zoezi hilo kuanza hapo Juni, 16, 2015.

Aidha, Kiongozi wa Mbio za Mwenge  Kitaifa, alikemea suala la rushwa akiwataka wananchi kuacha kupokea rushwa kwa kuwa inasababisha kuwapata viongozi wabovu.
 Pia, alisisitiza kutumia vyandarua kadri ya malengo ya serikali ili kupambana na malaria badala ya kutumia vyandarua hivyo kwa malengo tofauti.

Kuhusuna ugonjwa hatari wa Ukimwi, alisema  waliokwisha ambukizwa ugonjwa huo ni vema kuanza kutumia dawa za ARV na kula vyakura bora mapema na kufuata ushauri unaotolewa na madaktari.

Awali akipokea Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe. Rajabu Rutengwe alibainisha kuwa jumla ya miradi 51 itapitiwa na mwenge wa uhuru katika Mkoa wa Morogoro. “Mwenge  wa Uhuru ukiwa ndani ya Mkoa wa Morogoro utakimbizwa ndani ya Wilaya 6 ukipitia jumla ya miradi 51 yenye thamani ya shilingi 9,750,540,533.40” Alisema.

Aliongeza kuwa “kati ya hizo, michango ya wananchi ni shilingi,2,522,160,236.00, Halmashauri 574,640,680.00, Serikali Kuu 4,734,382,176.40.00 na wafadhili 1,919,357,441.00.

Mwenge wa Uhuru, kesho utaanza mbio zake Wilaya ya Gairo ambapo utapitia jumla ya miradi sita.

No comments:

Post a Comment