TANGAZO


Saturday, January 17, 2015

Mahafali ya Chuo cha Ufundi Arusha (ATC)

*Chakaribisha wawekezaji binafsi ujenzi wa Hosteli za wanafunzi wa kike
*Naibu Waziri Mhagama atunuku wahitimu 374 
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), wakiwa kwenye mahafali yao, ambayo Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenister Mhagama aliwatunuku wahitimu 374 Shahada mbalimbali.
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), wakiwa kwenye mahafali yao hayo. 
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), wakiwa kwenye mahafali hayo.
Wahitimu wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), wakiwa kwenye mahafali hayo. 
Baadhi ya wahitimu wa Chuo cha Ufundi Arusha (ATC), wakiwa kwenye mahafali yao.

Na Richard Mwangulube, Arusha
NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Jenista Mhagama(mb) leo ametunuku Astashahada, Stashahada na Shahada kwa wahitimu wapatao 374 katika chuo cha ufundi arusha—ATC.
Kati ya wahitimu hao 334 ni  wanafunzi waliohitimu astashahada na stashahada katika fani ya sayansi, teknolojia na uhandisi sanifu.
Aidha, wanafunzi 24 wamehitimu shahada katika  uhandisi ujenzi umwagiliaji, 13 wamehitimu   katika programu ya teknolojia Sayansi za maabara.
Aidha  wanafunzi 17 wamehitimu katika masuala ya ufundi sanifu uhandisi umeme na elektroniki.
Akizungumzia   program ya  ya teknolojia ya sayansi za maabara, Naibu Waziri Mhangama amesema program hii ni muhimu wakati huu serikali ya awamu ya nne  imeamua kujenga maabara  kwa ajili ya masomo ya sayansi katika kila shule ya Sekondari.
Naibu Waziri Mhagama amefafanua kwamba hivi sasa kuna upungufu mkubwa  wa wataalam wa eno hili katika shule zote za Sekondari.
Amesisitiza kwamba kuanzishwa kwa program hii na chuo cha ufundi Arusha itakwenda sanjali na makakati wa serikali  swa kujenga  maabara  katika shule zote za Sekondari hapa nchini.
Amesema kuna mahitaji makubwa ya watalaam  wa eneo hili katika shule zote za Sekondari nchini.
Amesisitiza kwamba  wataalam hawa wataweza kufundisha kwa vitendo masomo yote ya  sayansi  pamoja na kuvifanyia matengenezo  vifanyy hivyo pindi vikiharibika.

Pamoja na kutunuku rasmi astashahada, stashahada na shahada katika chuo hicho Naibu waziri huyo wa elimu na mafunzo ya ufundi amesema pia kuwa  wahandisi wa sayansi na teknolojia ni  muhimu katika karne hii ya mageuzi ya sayansi na teknolojia duniani.
Hata hivyo  Naibu Waziri Mhagama ametaka na kusisitiza kuwepo na uwiano  kati ya mafundi sanifu na wahandisi katika kuleta maendeleo  ya nchi na mageuziya uchumi nchini.
Amesema makundi haya mawili ni makundi ambayo yote hutegemeana katika utekelezaji wa kazi zao za kila siku za miradi ambapo bila  mafundi sanifu  wahandisi kamwe hawawezi kutekeleza miradi.
Amesema Tanzania bado inakabiliw ana upungufu mkubwa wa mafundi sanifu na wahandisi hasa katika kutekeleza uhandisi ujenzi na umwagiliaji katika sekta ya kilimo

Naibu Waziri huyo  amesema  uhandisi ujenzi na umwagiliaji  ni muhimu katika kupanua eneo  la umwagiliaji hapa Tanzania.
Hivyo chuo cha ATC  ni nguzo muhimu sana katika uendeshaji wa program hii hapa Tanzania ambapo program mbalimbali zinazotolewa na chuo hiki zinalenga kuwawezesha wahitimu kujiajiri.
Amepongeza jitihada zinazofanya   na chuo cha ATC katika kuendesha program mbalimbali  ambapo amesema  bado Tanzania kuna mahitaji makubwa ya mafundi sanifu kuwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera  ya maendeleo ya  elimu na mafunzo na ufundi.
Akizungumza wakati wa mahafali hayo Mwenyekiti wa bodi ya chuo hicho Abraham Nyanda amesema  program ya ufundi sanifu hasa ya uhandisi,sayansi na teknolojia na kilimo  zinamahitaji makubwa nchini. 
Mwenyekiti huyo  ameiomba serikali kuipa kipau mbele kwa kukiongezea raslimali fedha  chuo hicho.
Nyanda ametoa wito kwa wawekezaji binafsi kuwekeza katika chuo hicho  katika ujenzi wa mabweni na hosteli hususani  hosteli  na mabweni ya wanafunzi wa kike.

Hatua hii itakiwezesha chuo  kuchukua wanafunzi wengi wa kike  wapatao 500   wanaotimkiza vigezo wakati wa udahili ambapo hivi sasa wanafunzi wengi  w akike huachwa kutokana na umkosefu wa mabweni kwa ajili ya malazi.
Kwa upande  wake mkuu wa chuo hicho Dkt Richard Masika amesema  kati ya wanafunzi  374  waliohitimu mafunzo  leo kati yao  wahitimu 81 saw ana asilimia 21.7 ni wanafunzi wa kike.
Dkt Masika pia amesema kuwa  chuo kimepanga kuongeza udahili wa wanafunzi kutoka idadi ya sasa  ya wanafunzi 1,605  hadi  3,000  mwaka 2018/19.
Mkuu huyo wa chuo pia ameeleza katika hotuba yake  hiyo kwamaba Chuo kimepanga kuongeza program mpya kulingana na  mahitaji ya taifa na soko la ajira.
Amezitaja program zinazotarajiwa kuanzishwa  kuwa ni program ya Gesi na mafuta ambayo italenga kuwapa ujuzi wahitimu katika suala la usambazaji na matumizi sahihi ya bidhaa hiyo katika  jamii.
Program nyingine  ni ya  teknolojia ya sayansi za maabara za mahospitalini ambapo  chuo kwa mara ya kwanza chuo kimdto  wahitimu wa ufundi sanifu katika uhandisi umeme na vifaa vya tiba.

No comments:

Post a Comment