TANGAZO


Wednesday, December 3, 2014

Tanzania yaungana na Mataifa mengine kuadhimisha miaka 70 ya Usafiri wa Anga Duniani

Ofisa mwongoza ndege wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Bi. Mossy Kitangita akiwahamasisha baadhi ya vijana na wanafunzi waliotembelea banda la maonesho la kitengo cha kuongozea ndege (hawapo pichani) kusoma masomo ya Sayansi ili waweze kupata fursa ya kujiunga na fani ya uongozaji wa ndege ndani na nje ya nchi. (Picha zote na Aron Msigwa - MAELEZO)
Ofisa mwongoza ndege wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere  Bi. Mossy Kitangita (kulia) akimweleza Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaaban Mwinjaka  namna kitengo cha uongozaji wa ndege katika uwanja wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere kinavyofanya kazi na changamoto wanazokabiliana nazo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaaban Mwinjaka (Kushoto) akimuuliza swali Bw. Nyello Abeid, mkufunzi wa Chuo cha Usafiri wa Anga nchini kuhusu alipotembelea banda la maonesho la chuo hicho leo jijini Dar es Salaam wakati wa maadhimisho ya miaka 70 ya Usafiri wa anga duniani yanayoendelea nchini.
Meneja wa Huduma za Hali ya Hewa kwa Usafiri wa Anga kutoka Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) Bw. John Mayunga akifafanua utekelezaji wa majukumu ya Mamlaka ya Hali ya Hewa katika usafiri wa anga.
Mkuu wa masuala ya Ulinzi na Usalama katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Bw. Ole Laputi (kushoto) akitoa ufafanuzi kwa baadhi ya wananchi waliotembelea banda la maonesho la idara hiyo kuhusu baadhi ya vimiminika visivyoruhusiwa kwa abiria wanaotumia usafiri wa anga.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaaban Mwinjaka (Kushoto) akitembelea banda la maonesho la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kuona  utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa miundombinu na viwanja vya ndege  katika maeneo mbalimbali nchini.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) Bw. Charles Chacha akiongea na waandishi wa habari kuhusu hali ya usalama wa anga Tanzania na namna Tanzania ilivyofanikiwa kupunguza idadi ya ajali za ndege.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi Dkt. Shaaban Mwinjaka akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuhusu maadhimisho ya miaka 70 ya Usafiri wa anga duniani yanayoendelea nchini na namna Serikali kupitia Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) ilivyojipanga kuhakikisha usalama wa ndege na abiria wanaotumia anga la Tanzania.

No comments:

Post a Comment