TANGAZO


Sunday, November 30, 2014

Wanafunzi wa Kitivo cha Uhandisi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COET) Kampasi ya Kijitonyama waelimishwa kushiriki shindano la App star

Wanafunzi wa Kitivo cha Uhandisi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COET), Kampasi ya Kijitonyama wakimsikiliza kwa makini mmiliki wa mtandao wa Popote Media, Gillbart Mlaseko (kushoto), alipokuwa akiwafafanulia jambo kuhusu shindano la AppStar linaloendeshwa na Vodacom Tanzania linalohusu ubunifu wa program za simu za mkononi. Washindi watajishindia zawadi mbalimbali zikiwemo pesa taslim na safari za kwenda nchini India na Barcelona kushiriki katika shindano hilo ngazi ya Kimataifa. Wapili kushoto ni Meneja Uhusoiano wa Nje wa Vodacom Tanzania, Abigail Ambweni. 

Mmoja wa wanafunzi wa Kitivo cha Uhandisi cha Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COET), Kampasi ya Kijitonyama akimuuliza swali mshindi wa shindano la App Star mwaka 2012, Ernest Mwalusanya kuhusu na shindano la AppStar linaloendeshwa na Vodacom Tanzania linalowalenga wabunifu wa program za simu za mkononi ambapo washindi  watajishindia zawadi mbalimbali, zikiwemo pesa taslim na safari za kwenda nchini India na Barcelona kushiriki katika shindano hilo katika ngazi ya Kimataifa.
Mshindi wa shindano la AppStar mwaka 2012 Ernest Mwalusanya, akiwafafanulia jambo baadhi ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Kitivo cha Sayansi ya Kompyuta kuhusu jinsi ya kushiriki katika shindano la AppStar, linaloendeshwa na Vodacom Tanzania. Shindandano hilo ni mahususi kwa wataalamu wabunifu wa kutengeneza mobile applications. Washindi watajishindia zawadi mbalimbali, zikiwemo pesa taslim na safari za kwenda nchini India na Barcelona kushiriki katika shindano la ngazi ya Kimataifa. (Picha zote na mpigapicha wetu)

No comments:

Post a Comment