Rais Kikwete, akitoka katika Hospitali ya Johns Hopkins iliyoko Marekani, akisindikizwa na Daktari aliyemfanyia upasuaji wa tezi dume baada ya kupata nafuu.
Rais Kikwete, akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Marekani, Balozi Mula Mula na baadhi ya Maofisa wa ubalozi huo, walipomtembelea kumjulia hali alipokuwa hotelini wakati akiendelea kujiuguza jeraha la upasuaji wa tezi dume.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete atarejea
nchini kesho mchana, Jumamosi, Novemba 29, 2014 kutoka kwenye matibabu nchini
Marekani.
Mhe.
Rais atawasili Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, Dar Es Salaam, kwa ndege ya
Shirika la Ndege la Emirates saa 9:20 mchana.
Tunakaribisha
vyombo vya habari kuwepo Uwanjani kwa ajili ya ujio wa Mhe. Rais. Tunashauri
tuwe tumefika Uwanjani saa 8:30 mchana.
ASANTENI
IMETOLEWA NA:
KURUGENZI
YA MAWASILIANO YA RAIS,
IKULU – DAR ES
SALAAM.
28
NOVEMBA,2014
No comments:
Post a Comment