TANGAZO


Sunday, September 28, 2014

Wizara ya Habari yatakata SHIMIWI Morogoro

Wachezaji wa Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo wakijifua kabla ya kuanza mechi yao leo dhidi ya timu ya Polisi leo uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Baadhi ya mashabiki wakifuatilia mchezo wa mpira wa pete kati ya Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo na Polisi leo mjini Morogoro.


Na Eleuteri Mangi- MAELEZO
28/09/2014
SHAMRASHAMRA za mashindano ya  Shirikisho la Michezo ya watumishi Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) zimepamba moto kwa timu mbalimbali kumenyana katika michezo mjini morogoro.
Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo leo wameanza vema mashindano hayo kwa kuwapa kichapo timu ya Polisi kwa mchezo wa mpira wa pete kwa kuwachapa magoli 45 kwa 01 dhidi ya wapinzani wao na kuibuka washindi katika mechi hiyo.
Ushindi huo umetiwa hamasa ambapo wachezaji hao wanatambua kuwa Wizara hiyo ndio yenye dhamana ya kusimamia michezo nchini.
Wakicheza kwa umahiri, huku wakitambua kuwa wao ndio wanaopaswa kutoa mfano kwa timu nyingine zinazoshriki mashindano hayo,wacheaji hao walizitumia idara zote katika mchezo huo kikamilifu hivyo wailioibuka kidedea katika mchezo huo.
Akizungumzia ushindi wao Nahodha wa timu ya Wizara ya Habari, Vijana Utamaduni na Michezo Johari Kachwamba amesema kuwa siri ya ushindi huo ni nidhamu na kuzingatia maelekezo ya mwalimu na mazoezi wakati wote wa maandalizi ya mashindano hata wakati wa mashindano yanayoendelea.
Kachwamba amesema kuwa wanaendelea kujifua na hawabweteki na ushindi huo walioupata leo kwani mashindano mashindano ndio yanaanza.
Aidha, timu ya kuvuta kamba wanaume ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo imeshinda baada ya timu ya RAS Tanga kutokutokea uwanjani hapo, hivyo kujihakikishia nafasi ya kusonga mbele katika hatua inayofuata.

Mechi zilizochezwa leo uwanja wa Jamhuri Morogoro ni pamoja na kuvuta kamba wanawake kwa wanaume, mpira wa pete, na mpira wa miguu ambapo mwaka huu timu 54 zinashiriki mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment