TANGAZO


Sunday, September 28, 2014

Timu ya Ikulu yajiimarisha SHIMIWI 2014

Wacheaji wa timu ya Ikulu wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wao kabla ya mchezo wao kwnye mashindano ya SHIMIWI dhidi ya timu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo leo katika mchezo uliochezwa katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mjini Morogoro.
Wacheaji wa timu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiwa katika picha ya pamoja na mwalimu wao kabla ya mchezo wao kwenye mashindano ya SHIMIWI mwaka huu dhidi ya timu ya Ikulu leo katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), mjini Morogoro.
Mchezaji wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Abubakari Kombo akiwa na mpira na kujaribu kutoka mchezaji wa timu ya Ikulu aliyevalia jezi  namba. 16 Erick Kafuku wakati wa mechi  iliyochezwa leo katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mjini Morogoro. (Picha na Eleuteri Mangi- MAELEZO)

Na Eleuteri Mangi-MAELEZO
28/09/2014
MWALIMU wa timu ya Ikulu inayoshiriki mashindano ya Shirikisho la Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI) George Mbilinyi amewapongeza wachezaji wa  timu yake ya mpira wa miguu,  benchi lao la ufundi na  washabiki kwa kufanikisha ushindi wao muhimu katika mashindano hayo.

Timu ya  Ikulu ilianza mchezo vizuri kipindi cha kwanza na cha pili na kuwapelekea hadi mwisho wa mchezo kuwashinda Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kwa mabao 2-0 katika mchezo uliochezwa leo katika viwanja vya  Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) mjini Morogoro.

Mbilinyi amesema kuwa  ushindi huo umetokana na ushirikiano kutoka kwa  wachezaji walioonesha kiwango kikubwa katika mchezo huo wakiongozwa na kiwango cha kujituma uwanjani.

Mbilinyi amesema kuwa mpira wa miguu ni mchezo wa makosa, wapinzano wao walikosea na wao wakatumia nafasi hiyo kupata ushindi huo mnono wa mechi ya kwanza.

Naye Nahodhaa wa timu ya Ikulu Amos Ndege amesema kuwa mchezo huo umewapa hamasa na nguvu ya kujiandaa na mchezo wao unaofuata ili waendelee kufanya vizuri zaidi.

Aidha, Ndege amesema kuwa uwanja waliotumia unachangamoto kubwa kwani unahitaji kuandaliwa vizuri kwa ajili ya mashindano hayo muhimu kwa ajili ya kujenga afya bora za watumishi wa Serikali na watumiaji wengine wa uwanja huo.

Kwa upande wake Mwalimu wa timu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na MichezoTunge Shem amesema kuwa wanaendelea na maandalizi ya mchezo unaofuata na anayafanyia kazi makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa kwanza ili waweze kuibuka kidedea katika mchezo unaofuata.
Vilevile Nahodha wa timu ya Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Carlos Mlinda amesema kuwa wachezaji wa timu yake wote wapo fiti kukabiliana kesho na timu ya RAS Simiyu.

Mashindano ya SHIMIWI taifa ya mwaka huu ni ya 34 tangu kuasisiwa kwake ambapo mkoa wa Morogoro umekuwa mwenyeji mara kwa ya tatu miaka ikiwapo mwaka 2009, 2011 na mwaka huu.

No comments:

Post a Comment