TANGAZO


Thursday, September 18, 2014

Baraza la ushindani: Tutumieni kwa manufaa ya Taifa na ustawi wa uchumi nchini


Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa Baraza la Ushindani (FCT), Nzinyangwa Mchany, akifafanua jambo kwa waandisha, wakati alipokuwa akizungumza kuhusu madai ya aina za rufaa zinazosikilizwa na baraza hilo, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Ofisa Sheria Mwandamizi wa FCT, Hafsa Said. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa kwenye mkutano huo, wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa Baraza la Ushindani (FCT), Nzinyangwa Mchany (hayupo pichani), wakati alipokuwa akifafanua jambo kuhusu madai ya aina za rufaa zinazosikilizwa na baraza hilo.
Wapigapicha wa Televisheni, wakiwa kazini wakati wa mkutano huo na Maofisa wa Baraza la Ushindani nchini jijini leo.
Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa Baraza la Ushindani (FCT), Nzinyangwa Mchany, akifafanua jambo, wakati alipokuwa akizungumza kuhusu madai ya aina za rufaa zinazosikilizwa na baraza hilo, Dar es Salaam leo. Kushoto ni Ofisa Sheria Mwandamizi wa FCT, Hafsa Said.
Ofisa Sheria Mwandamizi wa Baraza la Ushindani (FCT), Hafsa Said, akifafanua jambo wakati wa mkutano huo na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa baraza hilo la Ushindani (FCT), Nzinyangwa Mchany.
Baadhi ya waandishi wa habari, wakimsikiliza Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi wa Baraza la Ushindani (FCT), Nzinyangwa Mchany (hayupo pichani), wakati alipokuwa akifafanua jambo kuhusu madai ya aina za rufaa zinazosikilizwa na baraza hilo.


Na Hassan Silayo-MAELEZO
Baraza la ushindani limewataka wananchi kulitumia Baraza hili kwa manufaa ya Taifa na ustawi wa uchumi nchini.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uchumi Nzinyangwa Mchany wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam.
“Baraza la ushindani lipo kwa ajili ya watu wote hivyo wananchi hawana budi kulitumia kwa manufaa ya Taifa”. Alisema Nzinyangwa.
Aidha, Nzinyangwa alisema kuwa baraza la ushindani ni chombo maalum cha rufaa za maamuzi au amri za Tume ya Ushindani na mamlaka za udhibiti kwenye sekta za Miundombinu,huduma za maji na nishati.
Pia alisema kuwa kesi zinazosikilizwa kwenye baraza zinahakikisha uzingatiaji wa misingi ya udhibiti ili kuleta umakini katika kusimamia sekta husika na ushindani wa haki sokoni.
Akizungumzia kuhusu rufaa zilizowahi kusikilizwa na baraza hilo Nzinyangwa alisema kuwa rufaa zinazosikilizwa na baraza la Ushindani zimegawanyika katika makundi manne.

Akizitaja rufaa hizo Nzinyangwa alisema ni rufaa kati ya mtoa huduma na mlaji, hii ni pale mlaji anapopewa huduma mbovu au hafifu kwenye sekta inayosimamiwa na mdhibiti kama maji, simu, nishati ya umeme pamoja na bidhaa za mafuta ya nishati.

Pia kuna aina ya rufaa kati ya wauzaji wawili wa bidhaa ya aina moja ama mbadala wake kama kampuni za usafirisha au kampuni za simu ambapo shauri hili litapelekwa kwa mdhibiti wa sekta husika na iwapo upande mmoja hautaridhika na uamuzi unahaki ya kuombea rufaa uamuzi huo kwenye baraza la ushindani.

Akiendelea kutaja Rufaa hizo Nzinyangwa alisema kuwa pia ipo rufaa kati ya mtoa huduma na mdhibiti wa sekta na hii ni pale mdhibiti wa sekta anapoandaa utaratibu wa kudhibiti  sekta na ikiwa mdau anaona utaratibu huo hautoshelezi au haukufuata sheria mdau ana haki ya kuwasilisha malalamiko kwenye chombo kilichotoa uamuzi huo.
Pia mdau wa soko anaweza kukata rufaa kwenye Baraza la ushindani ikiwa tume ya ushindani imetoa amri kwenye soko au kutunga kanuni Fulani juu ya utaratibu kuhusu usimamizi wa ushindani kwenye soko ambao mdau anaona uamuzi huo haukuwa sawa.
  Tume ya ushindani ina jukumu la kukataza uzalishaji na uuzaji wa bidhaa bandia sokoni,katika jukumu hilo maamuzi hayo yanaweza kukatiwa rufaa na mdau kwenye Baraza la Ushindani

No comments:

Post a Comment