Mkuu
wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akifungua kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linalofanyika
leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Kongamano hilo limejumuisha wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini
na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na gesi na vyama vya siasa.
Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (hayupo pichani) wakati akifungua kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linalofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Wakuu
wa mikoa ya Mbeya Abbas Kandoro (katikati) na Lindi Ludovick Mwananzila(
kushoto) na Mjiolojia Mwandamizi kutoka Idara ya Nishati Adam Zuberi (kulia) wakisikiliza
mada ya rasimu ya sera ya Petrol iliyokuwa inatolewa
leo katika kongamano la siku moja la
kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu hiyo
lililofanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini
Dar es Salaam.
Kamishna wa Nishati Eng. Hosea Mbise akiwasilisha mada kuhusu rasimu ya sera ya Petroli kwa wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na gesi na vyama vya siasa wakati wa kongamano la kupata maoni ya wadau linalofanyika leo katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam.
Kamishna
wa Nishati Eng. Hosea Mbise (kushoto) akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro mara
baada ya kufungua kongamano la siku moja
la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu
ya sera ya Petroli linayofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi
ya wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na
gesi na vyama vya siasa wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (hayupo
pichani) wakati akifungua kongamano la
siku moja la kupata maoni ya wadau
kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linayofanyika jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa mafuta na gesi, wabunge, viongozi wa dini na mikoa iliyofanyiwa utafiti wa mafuta na gesi na vyama vya siasa wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (hayupo pichani) wakati akifungua kongamano la siku moja la kupata maoni ya wadau kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linayofanyika jijini Dar es Salaam.
Waandishi
wa mkutano (Rapporteur) wakiandika taarifa mbalimbali wakati wa kongamano la
siku moja la kupata maoni ya wadau
kuhusu rasimu ya sera ya Petroli linayofanyika leo katika ukumbi wa
mikutano uliopo Hoteli ya New Africa jijini Dar es Salaam. (Picha zote na Anna
Nkinda- Maelezo)
Na Anitha Jonas –
Maelezo
TANZANIA imegundua
gesi asilia katika maeneo 19 ya mwambao
na kina kirefu cha maji baharini ambayo ina ujazo wa trilioni 50.5.
Kati ya maeneo
hayo 19 yaligundulika gesi hiyo ,matano yanapatikana katika mwambao na
14 yapo katika kina kirefu cha maji baharini .
Hata hivyo gesi
iliyogundulika katika maeneo ya mwambao kama Songo songo na Mnazi Bay kwa sasa
inatumika kufua umeme na pia kwa ajili ya matumizi ya viwandani,majumbani na
kwenye magari.
Hayo yamesemwa leo na Mkuu
wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro wakati akifungua kongamano la wadau wa mafuta
na gesi linalofanyika katika ukumbi wa mikutano uliopo Hoteli ya New Africa
jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa huyo amewataka
wadau hao watumie muda wao kutoa maoni yatakayosaidia kuwa Sera ya Mafuta na Gesi
asilia itakayowanufaisha watanzania pindi itakapoanza kutumika.
Kandoro ameongeza kuwa
ni vema Sera hiyo ikasaidia Serikali kupata mapato yake yatakayotokana na
Mafuta na Gesi asilia kwa ajili ya kuleata maendeleo mbalimbali kwa manufaa ya
wananchi wake.
“Uandaaji wa sera hii ulipitia
marejeo ya nyaraka mbalimbali ikiwemo sera ya petroli za nchi zilizogundua nishati
ya mafuta na gesi asilia zikiwemo
Uganda,Ghana,Sierra Leone na Pakistani”.
Mpaka Oktoba mwaka jana
(2013) Serikali ilikuwa imekamilisha sera ya gesi asilia ,hii ni kwa ajili ya
kutoa muongozo wa kusimamia na kuendesha biashara ya gesi asilia katika uchakataji,usafirishaji na usambazaji”, alisema Kandoro.
Amesema kuwa Sera
hiyo itazingatia na kuangalia kwa ukaribu suala la udhibiti wa mazingira ukomo
wa uzalishaji wa rasilimali hiyo pale utakapoanza.
Kwa upande wake Mkuu wa
Kitengo cha Jiolojia kutoka Wizara ya
Nishati na Madini Adam Zuberi amesema lengo
la sera hiyo ni kuhakikisha rasilimali ya gesi asilia inawanufaisha watanzania
wote kwa mapato yatakayopatikana katika
maeneo husika kwani asilimia 3 itabaki
Halmashauri kwa matumizi ya wananchi.
Naye Mwenyekiti wa
Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba
ameishauri Serikali kuwa makini katika makubaliano na makampuni yatakayochimba
gesi katika mgawanyo wa mapato kama inavyoonyesha katika sera kuwa asilimia 60
ya mapato itapelekwa Serikalini. Pia umakini na uangalifu wa hali ya juu unahitajika
kwenye makubaliano hayo.
Mkutano huo wa wa siku
moja uliandaliwa na wizara ya Nishati na Madini na kujumuisha wataalam mbalimbali waliobobea katika masuala
ya mafuta ,wawakilishi wa ofisi za ubalozi zilizopo nchini ,Vyama vya siasa ,
viongozi wa dini, Wakuu wa Mikoa na
asasi za kiraia.
No comments:
Post a Comment