TANGAZO


Monday, August 4, 2014

TAMASHA LA KUTOA ELIMU YA ATHARI ZA DAWA ZA KULEVYA KUFANYIKA SEPTEMBA DAR.



Na Winner Abraham-MAELEZO-Dar es salaam

UONGOZI  wa  ZION SOUNDS  umeandaa tamasha la kuelimisha jamii kuhusu athari za dawa ya kulevya  linatarajia kufanyika mapema mwezi ujao.


Tamko hilo limetolewa na Mtendaji Mkuu wa ZION SOUNDS  Bw. Junior Zion wakati wa mkutano na waaandishi wa habari  leo  jijini Dar es Salaam.

Amesema kuwa wameamua kuandaa tamasha hilo ili liweze kuwaelimisha  vijana kuacha  kujiingiza katika utumiaji wa dawa za kulevya.

“Kama tunavyojua kuwa vijana ndio viongozi wa baadaye hivyo wanahitaji msaada mkubwa katika makuzi na kuelimishwa ni jinsi gani wataepukana na janga hili hivyo wahamasishwe kwa njia tofauti tofauti”amesema Zion.

Ameongeza kuwa kwa takwimu za nyuma kidogo karibu ya asilimia 40% ya vijana tayari wanatumia dawa za kulevya  kama Cocaine na bangi.

Naye Meneja Matukio wa Zion Sounds Bi.Careen Dora  Bi Careen ametaja sababu zinazochangia vijana wengi  kujiingiza katika matumizi ya dawa na  pombe kuwa ni kama kutaka kujua kwani kipindi cha ujana ni kipindi ambacho wengi hutaka kujua vitu vingi  ambavyo ni vigeni kwao.


Amesema kuwa vijana wanaoanza kutumia pombe wakiwa na umri wa miaka 15 wanaathirika mara 5 zaidi wanapofikia umri mkubwa.

No comments:

Post a Comment