TANGAZO


Friday, August 29, 2014

Matukio katika picha Bunge Maalum la Katiba leo 29 Agosti, 2014 Mjini Dodoma


Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Mhe. Samia Suluhu Hassan (aliyebeba mkoba) akiwasili Bungeni kuendelea na majukumu ya Bunge Maalum la Katiba. Aliyemtangulia mbele ni Mkuu wa Idara wa shughuli za Bunge John Joel.


Mwakilishi wa Watanzania waishio Marekani ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Bw. Kadari Singo (kushoto), akifurahia jambo akiwa pamoja na waandishi wa habari leo 29 Agosti, 2014, viwanja vya Bunge, mjini Dodoma.


Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba, kulia ni Mhe. Stella Manyanya akiwa amefuatana na Mhe. Reuben Matango wakielekea ndani ya Bunge Singo leo 29 Agosti, 2014 Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma.



Mwakilishi wa Watanzania waishio Marekani ambaye pia ni Mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba, Bw. Kadari Singo (kushoto) akibadilishana mawazo na Mjumbe mwenzie, Mhe. Yusuph Singo  leo 29 Agosti, 2014 Bunge Maalum la Katiba mjini Dodoma. (Picha zote na Benedict Liwenga, Maelezo-Dodoma)

No comments:

Post a Comment