TANGAZO


Friday, June 27, 2014

Waziri Nyalandu azindua tovuti ya Kongamano la Ufugaji Nyuki Afrika mwaka 2014


Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Maimuna Tarishi akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Wazara hiyo kuzungumza na kuzindua tovuti ya Kongamano la Kwanza la Ufugaji Nyuki Afrika mwaka 2014 uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam leo.


Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akizungumza na hadhiri wakati wa uzinduzi wa Kongamano la Kwanza la Ufugaji Nyuki Afrika mwaka 2014 uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam leo.


Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu, akijisajili kushirikia kwenye tovuti ya Kongamano la Kwanza la Ufugaji Nyuki Afrika mwaka 2014, kama ishara ya kuzindua tovuti hiyo, shughuli iliyofanyika  kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam leo.Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maimuna Tarishi na Msemaji wa Wizara Nurdin Chamuya.

Baadhi ya washiriki wa uzinduzi huo, wakifuatilia uzinduzi wa tovuti hiyo.
 Baadhi ya washiriki wa uzinduzi huo, wakifuatilia matukio mbalimbali ya uzinduzi wa tovuti hiyo.
Waziri Nyalandu, akizungumza wakati wa uzinduzi wa tovuti hiyo, jijini Dar es Salaam leo.

Na Hussein Makame-MAELEZO
WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu amewataka wafungaji wa nyuki, wataalamu wa fani mbalimbali, watafiti, wafanyabiashara na wadau wengine kushiriki Kongamano la Kwanza la Ufugaji Nyuki Afrika mwaka 2014 litakalofanyika kuanzia Novemba 11 hadi 16 jijini Arusha.
Ametoa wito huo, wakati akizundua tovuti ya kongamano hilo kwenye ukumbi wa mikutano wa Kimataifa wa Julias Nyerere jijini Dar es Salaam leo na kuzikumbusha halmashauri za wilaya nchini ziwawezeshe wafugaji wa nyuki kutoka wilaya zao washiriki kongamano hilo.
“Wengi mnaweza kujiuliza kwa nini tunazindua, ni sahihi jibu kuwa:moja tunajivunia kwa kuandaa tukio muhimu kwa manufaa ya Afrika nzima katika kuendeleza ufugaji nyuki” alisema Waizari Nyalandu na kuongeza:
“Mbili tunaitangza Tanzania duniani kote kuwa maliasili tulizonazo yaani misitu na mapori yanatumika kwa kufuga nyuki; tatu Wizara ya Maliasili na Utalii inaandaa kongamano hili ili kuhamasisha ufugaji nyuki nchini”
Waziri Nyalandu alieleza sababu nyingine la kuandaa kongamano hilo ni heshima kwamba Tanzania inawajali wafugaji nyuki kwa kuwa ni kongamano la kwanza kufanyika Afrika na Tanzania.
“Nachukua fursa hii kuwaomba wafugaji nyuki, wataalamu wa fani mbalimbali, watafiti, waandishi wa habari, wafanyabiashara, wanafunzi na watendaji katika taasisi mbalimbali kushiriki kongamano hili” alibainisha Waziri Nyalandu.
Naye Katibu Mkuu wa wizara hiyo Maimuna Tarishi alisema tovuti ya kongamano ambayo ni http://www.apiafrica.org iliandaliwa na kuanza kutumika Februari mwaka 2014.
Aliongeza kuwa tuvuti hiyo inawezesha kupata taarifa muhimu za mahali litakapofanyika, kujiandikisha, kulipia banda la maonesho na ziara ya mafunzo, ambapo hadi sasa takriban washiriki 550 wakiwemo 250 kutoka nje ya nchi.
Alifafanua kuwa Wizara yake kwa kuzingatia uzoefu ilionao kwa kushiriki maonesho mbalimbali, iliona ni vyema kuandaa kongamano hilo ili kushirikisha wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya nchi kutoa mchango wa utafiti, teknolojia na kubadilishana uzoefu katika kuboresha, kutunza na kusimamia makundi ya nyuki kwa uzalishaji wenye wingi na ubora.
Kwa mujibu wa Afisa Nyuki Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Monica Kagya ada ya ushiriki kwa washiriki kutoka Tanzania ni Shilingi 100,000, mwanafunzi  Shilingi 20,000 na mshiriki kutoka nje ya nchi ni Dola 250.
     

  

No comments:

Post a Comment