TANGAZO


Monday, December 30, 2013

Mashambulizi ya risasi yatokea Congo


Milio ya risasi imesikika katika maeneo ya kituo cha Televishen ya taifa, makao makuu ya Radio na katika uwanja wa ndege.
Taarifa za polisi nchini humo zinasema vijana wenye mapanga na bunduki wamevamia maeneo hayo na kuwateka watangazaji wa vituo hivyo.
Watu walioshuhudia tukio hilo wameeleza kuwa milio ya risasi ilianzia katika uwanja wa kimataifa ambapo pia kuna taarifa kupitia mitandao ya kijamii pia milio ya risasi ilisika katika maeneo ya kituo cha jeshi.
Mashuhuda wanasema risasi zilizkuwa zikifyatuliwa kuelekezwa pande zote hivyo kuwalazimu watu waliokuwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa mjini Kinsasa kijificha kukwepa mashambulio hayo
Msemaji wa polisi Kanal Mwana Mputu anasema Polisi wanaendelea kudhibiti eneo hilo huku wakiendelea kuwasaka wanaohusika katika shambulio hilo japo hawaeleza sababu za shambulio hilo.

No comments:

Post a Comment