TANGAZO


Monday, December 30, 2013

Watoto wapotezana na wazazi Sudan Kusini


Mashirika ya misaada yamesema kuwa maelfu ya watoto nchini Sudan Kusini wanahofiwa kupotezana na wazazi wao kutokana na machafuko yanayoendelea yaliyoanza hivi karibuni nchini humo.
Shirika la Save the Children linasema kuwa idadi kuwa ya watoto wanaishi peke yao katika mazingira ya vijijini, ambapo kati yao wengine wazazi wao wameuawa mbele yao na nyumba zao kuharibiwa.
Katika mapigano yaliyochukua takriban wiki mbili zilizopita kwa mjibu wa shirika la Save the Children yalisababisha watu 1000 kuuawa ambapo watoto 60 katika eneo la Juba walikutwa wakiwa wametengana na familia zao anasema afisa wa shirika la Save the Children Helen Mould.
Zaidi ya watu 100,000 wameyakimbia makazi yao tangia kuanza kwa mapigano hayo huku familia pia zikisambaratika.Mashirika hayo ya misaada yanasema wakati watu wengine wakihifadhiwa katika makambi ya wakimbizi ama kuhifadhiwa katika jamii salama lakini bado watu wengine wakiwepo watoto walipatikana wakiwa wamejificha katika maeneo ya mabwawa ya maji huku wakinywa maji machafu.
Machafuko haya yaliyoanza kama mivutano ya kisiasa katika ya kiongozi wa waasi Riek Machar na Rais Salva Kiir yamechukua ukurasa mpya baada ya kuchukua sura ya mapigano ya kikabila.

No comments:

Post a Comment