TANGAZO


Friday, November 15, 2013

Ofisi ya Waziri Mkuu yaelezea Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi


Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya (katikati), akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Kushoto ni Kaimu Msemaji wa ofisi hiyo, Augustino Tendwa na kulia ni Ofisa habari wa Idara ya Habari, Maelezo, Fatma Salum. (Picha zote na Kassim Mbarouk-www.bayana.blogspot.com)
Baadhi ya waandishi wa habari, wakiwa kazini wakati Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya, alipokuwa akizungumza nao, jijini Dar es Salaam leo, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. 
Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Kushoto ni Kaimu Msemaji wa ofisi hiyo, Augustino Tendwa.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. 
Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Kulia ni Ofisa habari wa Idara ya Habari, Maelezo, Fatma Salum.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya, akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam jana, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Kushoto ni Kaimu Msemaji wa ofisi hiyo, Augustino Tendwa. Fatma Salum-Maelezo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya, akifafanua jambo kwa waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Kushoto ni Kaimu Msemaji wa ofisi hiyo, Augustino Tendwa. Fatma Salum-Maelezo.
Mkurugenzi Msaidizi wa Uwekezaji na Uwezeshaji, Ofisi ya Waziri Mkuu, John Mboya (katikati), akizungumza na waandishi wa habari, Dar es Salaam leo, kuhusu Utaratibu wa Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi. Kushoto ni Kaimu Msemaji wa ofisi hiyo, Augustino Tendwa na kulia ni Ofisa habari wa Idara ya Habari, Maelezo, Fatma Salum.



1.0UTANGULIZI
Maana ya Dhana ya PPP na Uzoefu wa Kimataifa


Ndugu Wanahabari, Dhana hii ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi inahusisha mikataba baina ya sekta ya umma na sekta binafsi ambapo sekta binafsi inahusika na kukarabati, kujenga, kuendesha, kutunza, au kusimamia mradi mzima au sehemu yake kulingana na vigezo maalum vya utendaji vilivyowekwa na sekta ya umma. Kwa utaratibu huu, sekta binafsi inabeba kwa kiasi kikubwa utekelezaji wa uwekezaji huo kwa muda fulani, kwa mategemeo ya kupata faida na malipo kulingana na mkataba husika. Kwa mfano, Serikali inaweza kuwa na mkataba na mwekezaji kujenga barabara yenye urefu wa km. 100 na yenye viwango fulani; na mwekezaji atatakiwa kusanifu, kujenga, kuendesha kwa gharama zake na hatimaye baada ya kurudisha mtaji wake na faida, anakabidhi mradi huo Serikalini.


Kimsingi ubia wa aina hii ni njia muafaka inayoweza kutatua matatizo yanayotokana na ukosefu wa fedha kuwezesha Serikali kusimamia, kuendesha na kutunza rasilimali  za umma kwa ufanisi. Faida za utaratibu wa PPP ni pamoja na kupunguza mzigo kwenye bajeti ya Serikali kutokana na kutumia ujuzi na ufanisi wa mwekezaji, hivyo kuiwezesha Serikali kuelekeza Raslimali zake kwenye miradi mingine ambayo utaratibu wa ubia hauwezekani.


Katika utaratibu wa PPP, Sekta Binafsi inabeba kwa kiasi kikubwa gharama zinazohusiana na ujenzi na uendelezaji wa mradi. Aidha, miradi tunayozungumzia hapa siyo ubinafsishaji wa mashirika ya umma ambapo Serikali inauza mali zake na Sekta Binafsi inakuwa na jukumu la kuendesha kwa faida. Miradi ya PPP tunayozungumizia hapa ni ile ambayo kimsingi ni jukumu la Serikali kuiendeleza, lakini kutokana na uchambuzi wa kina inaonekana kuwepo na uwezekano wa wawekezaji kuwekeza kwa faida. Mifano ya miradi hii ni kama vile ujenzi wa barabara, reli, viwanda vya ndege na huduma za kijamii kama vile huduma za afya na elimu.


Mataifa mbalimbali kama vile India, Malaysia, Korea, Marekani, Uingereza, Ujerumani, Australia, Chile, Brazili, Afrika Kusini na Lesotho  yanatumia utaratibu huu kutekeleza miradi kama vile barabara za kulipia (toll roads), usafiri wa reli, ujenzi na uendeshaji wa viwanja vya ndege, huduma za maji, ujenzi wa magereza, huduma za afya n.k. Kwa mfano, kwa upande wa Afrika Kusini na Lesotho wana  hospitali za kisasa na barabara za kulipia zinazoendeshwa kwa utaratibu wa PPP.  


2. SERA YA UBIA BAINA YA SEKTA YA UMMA NA SEKTA BINAFSI (2009)


Serikali yetu kama yalivyo Mataifa mbalimbali inakabiliwa na changamoto za upatikanaji wa Raslimali za kutosha za bajeti kuweza kutekeleza miradi na huduma za umma.  Mwaka 2009 Serikali iliandaa Sera ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi kwa lengo la kuweka mazingira wezeshi ya Kisera, Kisheria na Kitaasisi yenye lengo la kutoa fursa kwa sekta binafsi kushiriki katika ubia huo.


Sera inalenga kutoa miongozo ya ujumla kuhakikisha kuwa kama Taifa tunaandaa na kutekeleza miradi mizuri. Miongozo hii ni pamoja na mfumo wa sera mahususi, kisheria na kitaasisi;  upembuzi yakinifu unaozingatia masuala ya kiufundi, kiuchumi na kijamii; upatikanaji wa raslimali kutekeleza miradi ya PPP; mchakato wa ununuzi; mfumo wa mgawanyo wa vihatarishi (risk allocation); majadiliano ya mikataba; fursa za uwekezaji na uhamasishaji; kujenga ufahamu, kujenga uwezo na usambazaji wa teknolojia, utaratibu wa tozo, miradi ya ubia kwenye maeneo ya pembezoni na jitihada za uwezeshaji. 


3.SHERIA YA UBIA BAINA YA SEKTA YA UMMA NA SEKTA BINAFSI YA MWAKA 2010


Katika kutekeleza Sera hiyo, Serikali iliandaa Sheria ya Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ya mwaka 2010 ambayo imeweka mfumo wa kitaasisi wa utekelezaji wa miradi na huduma za ubia, pamoja na taratibu muhimu za kuzingatiwa. Kimsingi, Sheria imeanzisha Kitengo cha Uratibu wa miradi ya ubia chini ya Kituo cha Taifa cha Uwekezaji ambacho kina jukumu la kupokea, kuchambua na kuratibu miradi ya Ubia (PPP) kutoka kwenye Wizara, Idara, Wakala na Taasisi  za Serikali. Aidha, Kitengo cha Fedha chini ya Wizara ya Fedha kimeanzishwa kwa lengo la kuchambua masuala ya fedha kama vile mgawanyo sahihi wa athari zinazoambatana na mradi na athari kwenye bajeti ya Serikali. Mamlaka za Serikali zina jukumu kubwa la kufanya uchambuzi wa kina kuainisha na kutekeleza miradi kwa utaratibu wa PPP na kuiwasilisha kwenye Vitengo hivyo kwa ajili ya uchambuzi.


4.  KANUNI ZA UBIA BAINA YA SEKTA YA UMMA NA SEKTA BINAFSI YA MWAKA ZA MWAKA 2011


Kanuni za Ubia baina ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi za mwaka 2011 ziliandaliwa ili kubainisha taratibu mahususi za kuzingatiwa kuanzia utambuzi wa mradi, upembuzi yakinifu, mchakato wa ununuzi kumpata mwekezaji mahiri, kuandaa mkataba wa mradi na utekelezaji. Kimsingi Kanuni zinaeleza kwa kina vigezo vya kuzingatiwa kuhakikisha kuwa miradi na huduma za ubia zinaandaliwa kwa umakini kwa kuzingatia vigezo vya Sheria ya PPP. 


Kanuni zimebainisha kuwa upembuzi yakinifu wa mapendekezo ya miradi kutoka Sekta ya umma (solicited PPP Proposals) utafanywa na Mamlaka za Serikali na upembuzi yakinifu wa mapendekezo ya miradi inayoibuliwa na sekta binafsi itafanywa na sekta binafsi.  Vigezo vya kuzingatiwa katika kuandaa mapendekezo ya awali ya miradi hii pamoja na upitishwaji wake vimewekwa bayana. Kanuni pia zimeweka taratibu za uwasilishwaji wa upembuzi yakinifu kutoka ngazi ya Mamlaka za Serikali, Kitengo cha Uratibu hadi Kitengo cha Fedha. Aidha, Kanuni zimeweka utaratibu wa kufuatwa katika masuala ya zabuni, majadiliano na kusainiwa kwa mikataba.


4. Utekelezaji wa Sera ya PPP


4.1 Wizara na Mamlaka za Serikali zinaendelea na kuainisha na kufanya upembuzi yakinifu wa miradi ya PPP. Naomba nieleze kwa kifupi baadhi ya miradi ambayo Serikali inaendelea na maandalizi ya msingi ili itekelezwe kwa utaratibu wa PPP:


(i)                          Mradi wa Ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam-Chalinze (km 100) kuwa barabara ya haraka (Expressway) ambapo Wakala wa Barabara amekamilisha uandaaji wa upembuzi yakinifu wa awali (Prefeasibility Study).


(ii)                         Mradi wa Ujenzi wa Bandari Mpya ya Bagamoyo na Eneo Huru la Biashara (Portside Industrial Area) ambapo Serikali inashirikiana na mwekezaji kutoka China - China Merchant (Holding) International kutekeleza miradi hii. Serikali inaendelea na majadiliano na mwekezaji ili miradi hii ilete tija na manufaa kwa Taifa.


(iii)                Mradi wa Ujenzi wa Gati  Nne  (4) katika Bandari ya Mtwara ambapo taarifa ya Upembuzi yakinifu imewasilishwa kwenye Kitengo cha Uratibu.  Makadirio ya awali yanaonyesha mradi utagharimu dola za Kimarekani milioni 219.


(iv)               Mradi mpya wa Bandari ya Mwambani ambapo taarifa ya Upembuzi yakinifu inafanyiwa kazi.  Makadirio ya awali yanaonyesha kuwa mradi huu utagharimu dola za Kimarekani milioni 790.


Utekelezaji wa Sera ya PPP unahitaji sana wadau kujengewa uwezo. Kazi hii inatekelezwa na Mamlaka za Serikali na Sekta Binafsi. Ofisi ya Waziri Mkuu imeandaa na kutoa mafunzo kwa maofisa 60 walioteuliwa kusimamia utekelezaji wa miradi ya PPP.  Hapa niseme pia kuwa jambo la msingi ni kwamba utaratibu wa PPP hauna njia za mkato kwa kukwepa hatua za msingi kama vile kufanya uchambuzi wa kina.


Naomba nimalizie kwa kusema kuwa Serikali inafanyia marekebisho Sheria ya PPP kwa lengo la kuunganisha Vitengo vya PPP na kurahisisha michakato ya utekelezaji.  Kama mlivyosikia, ushirikishwaji wa sekta binafsi katika kutekeleza miradi hii ni muhimu sana katika kutekeleza mipango yetu ya maendeleo na niwaombe wote tuunge mkono jitihada za Serikali. 
Nawashukuru sana, ahsanteni kwa kunisikiliza.


Imetolewa na:
Idara ya Maendeleo ya Sekta Binafsi, Uwekezaji na Uwezeshaji,
Sehemu ya Uwekezaji,
Ofisi ya Waziri Mkuu


NOVEMBA 15, 2013

No comments:

Post a Comment