Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)Hiiti Sillo (kulia) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya mafanikio na changamoto wanazokutana nazo Mamlaka wakati wa utekelezaji majukumu yao hususani katika operesheni Giboia iliyofanyika tarehe 1 hadi 3 mwezi Oktoba mwaka huu nchini, kushoto ni Mkurugenzi wa Dawa na Vipodozi bwana Adam Fimbo.
Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishna Robert Manumba akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu taarifa ya matokeo ya operesheni Giboia iliyofanyika tarehe 1 hadi 3 mwezi Oktoba mwaka huu nchini.
Baadhi ya maofisa wa TFDA wakiwa katika mkutano huo.
Waandishi wa habari wakimfuatilia kwa makini Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishna Robert Manumba (hayupo pichani) wakati akitoa taarifa ya matokeo ya operesheni Giboia katika ofisi za Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) leo jijini Dar Es Salaam.
Baadhi ya dawa.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA)Hiiti Sillo (wapili kulia) akimuonesha dawa bandia zilizokamatwa wakati wa operesheni Giboia, Kulia ni Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishna Robert Manumba.
Msemaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) akieleza jambo kwa Mgeni Rasmi Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai Kamishna Robert Manumba jinsi Mamlaka ya Chakula na Dawa inavyotekeleza majukumu yake. (Picha zote na Eliphace Marwa-Maelezo)
No comments:
Post a Comment