Ofisa Mawasiliano Mwandamizi wa
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Bw. Luhende Singu (kushoto), akieleza kwa
waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhuasu mpango wa huduma za matibabu kwa
mama wajawazito na watoto kwa Mikoa ya Mbeya na Tanga, wakati wa mkutano uliofanyika
ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo, Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Ofisa
habari Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Frank Mvungi.
Ofisa Msimamizi wa Mradi huo, toka
Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Dk. Daudi Bunyinyiga akifafanua jambo kwa
waandishi wa habari (hawapo pichani), kuhusu faida na malengo ya mradi huo, aliyotaja kuwa ni kusaidia wanawake wajawazito na watoto wanaotoka
katika familia zisizo na uwezo ambao watalipia shilingi elfu kumi (10,000) kwa mwaka
ili kupunguza vifo vya akina mama wajawazito, wakati wa mkutano uliofanyika
ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) leo, Jijini Dar es Salaam. (Picha na Eliphace
Marwa-MAELEZO)
1.0
UTANGULIZI:
Historia
ya NHIF – Mfuko wa Taifa wa Bima ya
Afya (NHIF) ulianzishwa kwa Sheria Namba 8 ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na kuanza shughuli zake rasmi Julai 1, 2001.
2.0
UTEKELEZAJI WA MPANGO WA
KFW:
Pamoja
na majukumu mengine, NHIF imekuwa
ikishirikiana na wadau wa ndani ya nje ya nchi katika kutekeleza miradi mbalimbali
inayohusu afya. Hivi sasa NHIF kwa
kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya watu wa Ujerumani -KFW- inaendesha mradi
wa huduma za matibabu kwa Mama Wajawazito
wasio na uwezo na watoto katika mikoa ya Tanga na Mbeya. Hii ni kufuatia
makubalino yaliyofanywa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na
Serikali ya Ujerumani, ambao lengo lake ni kupunguza vifa vya mama wajawazito
na watoto nchini.
3.0
HISTORIA YA MPANGO WA KFW:
Mpango huu wa miaka mitatu umeanza utekelezwa mwezi
Februari mwaka 2012 na unatarajiwa
kukamilika mwezi Desemba mwaka 2014.
Mpango huu ambao unatekelezwa katika mikoa ya Tanga na
Mbeya unawapa fursa akina mama wajawazito wasio na uwezo kupata huduma ya upimaji
na matibabu bure ukilenga kupunguza vifo vya watoto wachanga na madhara mengine
ambayo yanawakabili wanawake wajawazito na watoto wao wachanga ili kufikia
malengo ya Milenia hususani namba 4 na 5.
4.0
SIFA ZA WANACHAMA:
Mwanachama au mnufaika wa mpango wa KFW ni mwanamke yeyote
mja mzito mkazi wa mkoa wa Mbeya au Tanga, ambaye amejaza fomu ya kujiandikisha
kupata huduma za vipimo na matibabu kupitia mpangp huu.
5.0
MUDA WA KUNUFAIKA NA MPANGO WA KFW:
Mama
mjamzito atanufaika na huduma za vipimo na matiba katika muda wote wa ujauzito
wake na miezi mitatu baada ya kujifungua. Baada ya miezi mitatu tangu
kujifungua mama wa mtoto na familia yake wanapatiwa kadi ya Mfuko wa Afya ya
Jamii (CHF) kwa kupitia mradi huu wa NHIF/KFW ya mwaka mmoja kwa mujibu wa
taratibu za matibabu za Halmashauri inayohusika.
Kadi hiyo inampa nafasi mama mwenye mtoto na familia yake (mumewe
na watoto wasiozidi wanne wenye umri wa chini ya miaka kumi na nane) kupata matibabu bure katika vituo vya matibabu ndani ya
Halmashauri husika.
MAFANIKIO
YA MPANGO WA KFW:
Hadi sasa familia 53,253 zinapata huduma za matibabu kupitia mpango huu, kati ya
lengo la familia 70,000 katika kipindi cha miaka
mitatu. Lengo tarajiwa hadi
kufikia tarehe 30 Septemba 2013 ilikuwa ni kusajili wanachama
40,834 ambayo ni sawa na asilimia 130 ya lengo tarajiwa.
GHARAMA
ZA UTEKELEZAJI:
Tangu kuanza kwa utekelezaji wa mpango huo kiasi cha Shilingi Bilioni 2,481,700,138.40/=
zimetumika ambapo kiasi cha Shilingi 1,145,367,000/= kimetumika kugharamia matibabu kwa familia za akina mama waliojiunga
na mpango huu na malipo kwa ajili ya kuwapatia kadi katika Mfuko wa Afya ya
Jamii – CHF.
Aidha kiasi cha Shilingi 347,204,780/= zimetumika kutoa elimu kwa umma kupitia redio,
vipeperushi, magazeti na kuandaa mifumo ya taarifa.
Pia Shilingi 989,128,358.40 zimetengwa kwa ajili ya kuboresha miundombinu kwa kununua
vifaa tiba kwa ajili ya vituo vya matibabu katika mkoa wa Tanga na Mbeya.
CHANGAMOTO
ZA MPANGO HUU:
1. Vituo vya kutolea huduma kuwa na upungufu wa dawa ambapo
walengwa wanalazimika kutembea mwendo mrefu ili kufauta huduma katika vituo
vilivyosajiliwa na NHIF.
2. Mwitikio mdogo wa watoa huduma katika kuwasilisha madai yao
baada ya kutoa huduma kwa kundi hili maalumu,
HITIMISHO:
NHIF inatarajia kuwa mpango huu utasadia kupunguza
changamoto zinazoikabili sekta ya afya hapa nchini katika kuhudumia wakina mama
wajawazito na kuwaweka katika mazingira salama ya kujifungua na kuwapa uhakika
wa huduma za matibabu, wao na watoto wao baada ya kujifungua.
Kauli mbiu yetu ni “Afya Bora Ndiyo Mambo Yote.”
No comments:
Post a Comment