TANGAZO


Thursday, May 30, 2013

Rais Dk. Shein atembelea Jimbo la Jiangsu nchini China, azungumza na wanafunzi wa Tanzania wanaosoma jimboni humo

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akifuatana na Makamo wa Rais wa Kampuni ya Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari (ZTE), Bi. Chen Jie, wakati alipotembelea Ofisi za kampuni hiyo, katika Mji wa Nanjing, Jimbo la Jiangsu, nchini China, akiwa katika ziara ya Kiserikali kwa mualiko wa Serikali ya Jamhuri ya Watu  wa China. (Picha zote na Ramadhan Othman, China)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein pamoja na ujumbe wake, wakipata maelezo kuhusu vifaa mbalimbali vya mawasiliano zikiwemo simu katika Ofisi ya Kampuni ya Teknolojia ya mawasiliano ya habari (ZTE), wakati alipotembelea Ofisi za kampuni hiyo leo,  akiwa  katika ziara ya Kiserikali kwa mwaliko wa Serikali ya Jamhuri ya Watu  wa China, katika Mji wa Nanjing, Jimbo la Jiangsu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na mkewe, Mama Mwanamwema Shein (katikati) pamoja na ujumbe wake, wakiwa na Mwenyeji wao, Makamo wa Rais wa Kampuni ya Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari (ZTE), Bibi Chen Jie (wa pili kushoto), wakiangalia simu na kupata maelezo ya matumuizi ya simu hizo, walipotembelea sehemu mbalimbali, wakiwa katika ziara ya Kiserikali kwa mwaliko wa kukuza ushirikiano katika nyanja za kiuchumi na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (kushoto), mkewe Mama Mwanamwema  Shein (wa pili) na Balozi Mdogo wa China, anayefanyia kazi zake Zanzibar, Bibi Chen QiMan, wakimsikiliza Dk. Dai Xuelong, wakati alipokuwa akiwaonesha baadhi ya vifaa vya mawasiliano, vilivyotengenezwa na Kampuni ya ZTE, alipotembelea Ofisi za kampuni hiyo, akiwa katika ziara ya Kiserikali nchini China katika Mji wa Najing, Jimbo la Jiangsu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na mkewe, Mama Mwanamwema Shein (katikati) pamoja na ujumbe wake, wakielekea katika chumba maalum cha Mitambo ya Teknolojia ya Mawasiliano katika Ofisi za Kampuni hiyo, Mjini Najing, Jimbo la Jiangsu nchini China, wakiwa katika ziara ya Kiserikali nchini humo leo.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na mkewe, Mama Mwanamwema Shein, wakiwa wamevalia vazi maalum, wakati walipoingia katika chumba cha Mitambo ya Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari, katika Ofisi za kampuni hiyo, Mjini Najing, Jimbo la Jiangsu nchini China, katika ziara rasmi ya Kiserikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na mkewe, Mama Mwanamwema Shein, wakiangalia Mitambo ya Teknolojia ya Mawasiliano, ikifanya kazi, walipotembelea katika Chumba Maalum cha Mitambo hiyo, Ofisi za kampuni hiyo, Mjini Najing, Jimbo la Jiangsu nchini China, katika ziara rasmi ya Kiserikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein na mkewe, Mama Mwanamwema Shein (katikati), wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Kampuni  ya Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari (ZTE), nchini China pamoja na ujumbe aliofuatana nao, mara baada ya kuwasili katika Ofisi za kampuni hiyo, huko katika Mji wa Nanjing, Jimbo la Jiangsu, nchini China akiwa katika ziara ya Kiserikali kwa mwaliko wa Jamhuri ya Watu wa China. 
Wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Elimu za Juu katika Vyuo Vikuu mbalimbali katika Mji wa Nanjing, Jimbo la Jiangsu nchini China, wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa  Sofitel Luxury Hotel, katika mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein.
Baadhi ya wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Elimu za Juu katika Vyuo Vikuu vya Mji wa Nanjing, Jimbo la Jiangsu nchini China, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (hayupo pichani), wakati alipozungumza nao  leo, ukumbi wa mikutano wa Sofitel Luxury Hotel, Mjini Nanjing katika jimbo la Jiangsu akiwa katika ziara  ya Kiserikali.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein (wa pili kushoto), akiwa na mkewe, Mama Mwanamwema Shein (kushoto) pamoja na Mawaziri na Maofisa aliofuatana nao katika ziara ya Kiserikali nchini China. Rais alipata muda wa kuzungumza na wanafunzi wa Tanzania wanaosoma Vyuo Vikuu mbalimbali na kuwaelezea  hali halisi ya utulivu na amani iliyopo nchini Tanzania na  kuwataka kuondokana na wasiwasi.

Mwanafunzi Sauli Elingarama, Daktari wa bianadamu, akiuliza  swali mbele ya Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, wakati wa mazungumzo na wanafunzi wa Tanzania wanaosoma, Vyuo Vikuu vya Mji wa Nanjing, nchini China katika Jimbo la Jiangsu. Rais yupo  China kwa ziara ya Kiserikali.

No comments:

Post a Comment