Mbunge kutoka Ghana, Alban Bagbin akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari, kuhusu umuhimu wa Mkutano wa Wabunge walio katika Mtandao wa Kimataifa wa Kutetea Amani, Maendeleo, Utawala wa Sheria na Haki za Binadamu duniani, watakavyopanga mikakati mbalimbali ya kuzishawishi nchi wanazotoka kusaini mikataba inayozuia uagizaji, uingizaji na usambazaji wa silaha katika nchi zao, kuyafikia makundi yasiyohusika ambayo yamekuwa chanzo cha uvunjifu wa amani duniani. Takribani wabunge 22 kutoka nchi za Afrika wanashiriki mkutano huo.
Mbunge kutoka Sierra Leone, Bernadette LAHAI, akiwaeleza waandishi wa habari (hawapo pichani), athari zinazosababishwa na silaha kuangukia katika mikono ya wahalifu hasa katika bara la Afrika na kuwa chanzo cha machafuko na kukwamisha maendeleo ya wananchi.
No comments:
Post a Comment