TANGAZO


Thursday, April 4, 2013

Waziri Samia atembelea Uhamiaji mjini Zanzibar leo

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano, Samia 
Suluhu Hassan akioneshwa aina mbalimbali za Passpoti ambazo zinatumika hapa nchini na Mkuu wa Kitengo cha Uzalishaji Passpoti na Ukazi, Haji Hamza Khamis, wakati wa ziara yake ya kutembelea Taasisi za Muungano, zilizopo Zanzibar leo. (Picha zote na Ali Meja)

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano Samia Suluhu Hassan  akionyeshwa vibali vya Ukazi nchini na Mkuu wa Kitengo cha kuzalishia Passpot na Ukazi, Haji Hamza wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi za Muungano, ziliopo Zanzibar leo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano, Samia Suluhu Hassan, akioneshwa vibali vya Ukazi nchini na Mkuu wa Kitengo cha kuzalishia Passpot na Ukazi, Haji Hamza wakati wa ziara yake ya kutembelea taasisi za Muungano ziliopo Zanzibar leo.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano, Samia Suluhu Hassan, akiuliza jambo kwa Kamishna wa Uhamiaji Zanzibar, Mwinchumu Hassan Salum, kwenye chumba cha kutunzia kumbukumbu za Nyaraka za kuzaliwa, wakati wa kuomba passpoti nchini.



Na Ali Issa- Maelezo Zanzibar, 4/4/2013.

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano, Samia Suluhu Hassan, amewataka Maofisa Uhamiaji wanaokusanya Mapato, kuwa waadilifu katika ukusanyaji wa mapato yatokanayo na huduma wanazozitoa hapa nchini, ili kuweza kujitatulia changamoto zinazowakabili.

Hayo ameyasema leo, huko katika Ofisi ya Uhamiaji Kilimani mjini Unguja wakati alipofanya Ziara ya kuitembelea Idara hiyo ikiwa ni mfululizo wa Ziara zake ya kuzitembelea Taasisi za Muungano zilizopo Zanzibar.

Amesma iwapo Maafisa hao watafanya kazi kwa uadilifu katika kukusanya Mapato wataweza kuzitatua changamoto zinazo wakabili katika idara yao na kupiga hatua mbele.

“Uadilifu unahitajika katika makusanyo ya fedha, kwani mnaweza kudai kupatiwa mengi na ikawezekana lakini kama hakuna makusanyo mazuri itakuwa viguma kuyapata mnayoyadai”alisema Samia.

Aidha waziri huyo alisema kuwa  iwapo uadilifu utaongezwa matatizo madogo madogo kama vile uchimbaji wa Kisima na Ufungaji wa Lifti katika Jengo jipya la Uhamiaji ni rahisi Maafisa hao kuufanya wenyewe ndani ya kipindi kifupi.

Waziri huyo aliwaeleza wafanyakazi hao kulifanyia kazi suala hilo pamoja na  kuwa na mashirikiano katika kazi na maamuzi wanayoyatoa yawe ya pamoja bila ya kuwa na malumbano.

Awali akimkaribisha Waziri Samia, Kamishna wa uhamiaji Zanzibar Mwichum Hassan Salum amemueleza waziri kuwa katika kuleta uadilifu wa ukusanyaji wa mapato Idara ya uhamiaji imeunzisha Kitengo kinachopambana na rushwa kwenye huduma zao.

 Amesema wameweka mfumo malumu katika Afisi zao kwa ajili ya kupokea kero na maoni ya wananchi kuhusu utendaji wa kazi zao.

Mwichumu alimueleza Waziri kuwa Idara hiyo inakabiliwa changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na uhaba wa watumishi 105 ambapo kwa sasa idadi ni Watumishi  375 ambao ni wa chache kutokana na majukumu kuongezeka.

Katika hatua nyingine Waziri Samia alitembelea idara ya Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Ofisi ya Zanzíbar na kuwasihi Watendaji wake kufanya kazi kwa mujibu wa sheria na uzalendo na bila kumpa mtu yetote asiyestahiki kitambulisho hicho.

No comments:

Post a Comment