Wachezaji wa Barack Young Controllers ya Liberia, wakitoka uwanjani leo asubuhi.
Wachezaji wa Barack Young Controllers ya Liberia, wakipanda basi la Hoteli wanayofikia leo asubuhi mara baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere leo. |
Kocha na wachezaji wakiwa ndani ya basi tayari kwa safari ya Hotelini leo asubuhi. |
Basi lililowabeba wachezaji wa timu hiyo ya Liberia, inayopambana na Azam FC Jumamosi hii, Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Mtoto wa Rais wa Liberia, Robert Alvin Sirleaf (kushoto), akiwa na mmoja wa viongozi, ambaye alikuwa kwenye msafara huo. |
Hoteli waliofikia wachezaji wa timu hiyo, jijini Dar es Salaam leo.
Wakishuka kwenye basi hilo na kuingia hotelini. |
Wakiwa ndani ya Saphirre Court Hotel, jijini Dar es Salaam leo. |
TIMU ya Barrack Young
Controllers II ya Liberia imetua leo asubuhi huku ikiwa na matumaini kibao ya
kuwafunga wapinzani wao Azam FC.
Naye kocha wa
timu hiyo, Robert Lartey, amejigamba kuwa
uwezo wa kuifunga Azam FC kwenye mchezo wa marudiano wa kombe la Shirikisho utakaochezwa jijini Dar es Salaam
jumamosi kwani makosa yaliyoigharimu timu amekwisha yafanyia
marekebisho
“Mchezo huu ni muhimu kwa
timu yangu na naamini nitashinda”, alisema Lartey.
Pia alijigamba kuwa na kikosi
chenye wachezaji wenye vipaji ambao pia wapo timu ya taifa ya Liberia ya Vijana,
akina Ezekiel Doe, Benjamin Gbamy na George Dauda.
Wachezaji wa timu hiyo
wameonekana kuwa nyuso zao kutokuwa na furaha sijui ni kwa kutafakari kuwa
walipoteza mchezo wa awali wakiwa nyumbani na sasa wanacheza
ugenini.
Young Controllers imetua leo
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 2:30 kabla ya muda wa
3.35 asubuhi ambao ulitarajiwa kwa ndege ya PrecisionAir ikitokea Nairobi, Kenya
inapounganisha safari hiyo inayoanzia Monrovia kupitia Accra,
Ghana.
Kocha huyo amesema hali ya
hewa ya Dar es salaam haijatofautiana sana na hali ya hewa ya Liberia jana
amekiri Dar es Salaam kuwa na joto kuzidi Monrovia
Msafara wa timu hiyo umetuwa
na watu 37, wachezaji 21 na unaongozwa na Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa klabu
hiyo Robert Alvin Sirleaf ambaye ni mtoto wa Rais wa Liberia, Ellen Johnson
Sirleaf, Samuel Sumo wakati Meneja wa timu ni Clarence Murvee. Daktari wa timu
ni Samuel Massaquoi.
No comments:
Post a Comment