TANGAZO


Tuesday, April 2, 2013

Sherehe za Maadhimisho ya Siku ya Mtoto Yatima Zanzibar



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali 

Mohamed Shein, akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa 

Taasisi ya Muzdalifa, Sheikh Abdalla Hadhal, alipokuwa akiangalia 

maonesho ya picha mbalimbali, wakati wa maadhimisho ya siku ya 

mtoto Yatima katika Ukumbi wa Salama Bwawani. Maadhimisho 

hayo, yamefanywa leo na Shirika la I.H.H la nchini Uturuki kwa 

ushirikiano  na Jumuiya ya Muzidalifa ya Zanzibar, inayoshuhulika 

na Yatima. (Picha zote na Ramadhan Othman, Ikulu)


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali 

Mohamed Shein, akipokea zawadi kutoka kwa mtoto Hinaina Said 

Khalfan, wakati wa sherehe za Siku ya Mtoto yatima zilizofanyika 

ukumbi wa Salama Bwawani Hotel leo,  Mjini Zanzibar. Hafla hiyo 

imeandaliwa na shirika la misaada la I.H.H la Uturuki, kwa 

Ushirikiano na Jumuiya ya Muzdalifa ya Zanzibar.

Watoto Yatima waliohudhuria katika sherehe za maadhimisho ya 

siku ya Mtoto Yatima, wakiwa katika Ukumbi wa Salama Bwawani, 

Mjini Zanzibar leo, katika sherehe zilizoandaliwa kwa ushirikiano  

na Jumuiya ya Muzdalifa na shirika la misaada la I.H.H la nchini 

Uturuki leo na kuhudhuriwa na wananchi na viongozi mbalimbali.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali 

Mohamed Shein, akipokea risala kutoka kwa Nasra Suleiman 

Abdalla, wakati wa sherehe za maadhimisho ya Siku ya Mtoto 

yatima zilizofanyika leo, katika ukumbi wa Salama Bwawani, mjini 

Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali 

Mohamed Shein, akitoa hutuba yake wakati wa Sherehe ya 

maadhimisho ya Siku ya Mtoto Yatima katika ukumbi wa Salama 

Bwawani Hoteli, mjini Zanzibar leo. Maadhimisho hayo, 

yamesimamiwa na Jumuiya ya Muzidalifa na Shikika la misaada la 

I.H.H la nchini Uturuki. Kushoto ni Makamo wa Kwanza wa Rais 

wa Zanzibar, Maalim Seif Sharif, Balozi wa Uturuki, nchini Ali 

Daudi Gul na Kulia ni Waziri wa Katiba na Sheria, Abubakar 

Khamis Bakary.

No comments:

Post a Comment