TANGAZO


Friday, December 14, 2012

Wafanyakazi Bora wa mwaka 2012, Wizara ya Fedha wapewa tuzo

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma (kushoto), akipokea tuzo ya ufanyakazi bora wa kitengo kutoka kwa Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa katika tafrija fupi ilifanyika jana jijini Dar es Salaam kufuatia kuchaguliwa kwake mwezi Mei mwaka huu kuwa mfanyakazi bora wa mwaka 2012.



Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Fedha Ingiahedi Mduma (kushoto), akikabidhiwa tuzo yake ya ufanyakazi bora wa kitengo na Waziri wa wizara hiyo, Dk. William Mgimwa katiaka tafrija iliyofanyika jana wizarani hapo. 


Mkuu wa Mfuko wa Mikopo wa Hazina kutoka Idara ya Mhasibu Mkuu wa Serikali, Wizara ya Fedha, Christina Ngonyani, akipokea tuzo ya ufanyakazi bora wa kitengo kutoka kwa Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa (kulia), katika tafrija fupi ilifanyika jana jijini Dar es Salaam kufuatia kuchaguliwa kwake kuwa mfanyakazi bora kwa mwaka 2012.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhan Khijjah (kushoto), akipongezwa na Waziri wa Wizara hiyo, Dk. William Mgimwa (kulia), baada ya kuwa mmoja wa wafanyakazi bora wa Wizara kwa mwaka 2012, wakati wa hafla fupi ya kuwapa tuzo wafanyakazi hao, iliyofanyika jana jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wafanyazi mbalimbali.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ramadhan Khijjah, akipokea tuzo ya ufanyakazi bora wa Wizara hiyo, kutoka kwa Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa (kulia), katika tafrija fupi ya kuwazawadia wafanyakazi bora, ilifanyika jana jijinii Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wafanyazi mbalimbali wa wizara hiyo.

Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa (katikati), akizungumza wakati alipokuwa akiwapongeza wafanyakazi bora wa Wizara ya Fedha waliochaguliwa mwezi Mei mwaka huu kuwa wafanyakazi bora kwa mwaka 2012 wakati wa tafrija fupi ya kuwazawadia ilifanyika jana mjini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na wafanyazi mbalimbali.
 
Waziri wa Fedha, Dk. William Mgimwa (wa pili kushoto), Katibu wa Wizara ya Fedha, Ramadhan Khijjah (wa kwanza), wakishirikiana na viongozi wa Chama cha Wafanyakazi cha TUGHE na wafanyakazi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam, wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa tafrija fupi jana ya kuwapongeza wafanyakazi bora  wa mwaka 2012. (Picha zote kwa hisani ya Wizara ya Fedha)

No comments:

Post a Comment