TANGAZO


Saturday, December 15, 2012

FM Academia yasherehekea miaka 15 tangu kuanzishwa kwake


Rais wa bendi ya FM Academia, Nyoshi El Saadat ( wa pili kushoto) na waliokuwa Wakurugenzi wa bendi hiyo, miaka ya nyuma Abas Mwinyi 'Sadamu Hussein' (kushoto) na Felician Chaula (wa tatu kushoto) pamoja na warembo mashabiki wa bendi hiyo, wakikata keki kwa pamoja,  wakati wa kusherehekea kutimiza miaka 15 ya huduma yake katika kutoa burudani nchini Tanzania, iliyofanyika kwenye klabu ya Msasani jijini Dar es Salaam na kuambatana na onesho kubwa na la kukata na shoka lililoshirikisha mashabiki, wadau na watu mbalimbali wa karibu na bendi hiyo.
Onesho la bendi ya FM Academia kutimiza miaka 15 tangu kuanzishwa kwake nchini  linadhaminiwa na Kampuni ya simu za mkononi ya Tigo.

Wakurugenzi wa bendi hiyo miaka ya nyuma Abas Mwinyi 'Sadamu Hussein' (wa tatu kushoto) na Felician Chaula (wa nne), pamoja mashabiki, wakifungua shampeni wakati wa hafla hiyo.
Keki maalum iliyoandaliwa kwa ajili ya hafla ya maadhimisho ya miaka 15 ya bendi hiyo.
Mwanamuziki Jose Mara wa bendi ya Mapacha Watatu. ambaye pia aliwahi kuwa mwanamuziki wa bendi ya FM Academia, akifanya vitu vyake na bendi yake katika maadhimisho hayo.
Vimwana wa bendi ya Mapacha Watatu wakifanya vitu vyao jukwaani katika maadhimisho hayo.
Hapa mzuka wa muziki umepanda na uko juu sana kama unavyoonekana, wacheza shoo, wakiwajibika vilivyo jukwaani.
Baadhi ya mashabiki wa bendi hiyo, hawakuwa nyuma kulisakata Sebene la FM Academia kama wanavyoonekana.Vijana wa FM Academia, wakifanya vitu vyao jukwaani usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Msasani Club, jijini Dar es Salaam.
Vijana wa FM Academia, wakifanya vitu vyao jukwaani usiku wa kuamkia leo kwenye ukumbi wa Msasani Club jijini Dar es Salaam.
Vimwana wa bendi ya FM Academia, wakionesha uwezo wao katika kucheza mambo ya Nzombo na Matembele.
Mashabiki wa bendi hiyo wakijimwaga stejini, wakati bendi hiyo ikipiga muziki katika ukumbi wa Msasani Club, jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo. (Picha zote kwa hisani ya Fullshangwe blog)


Wapiga vyombo (magita) wa bendi hiyo, waking'uta vyombo hivyo, wakati bendi ilipokuwa ikitumbuza katika onesho hilo.
 
Mashabiki wa bendi hiyo, wakijimwaga stejini, baada ya kupandwa na mdadi wa midundo ya  bendi hiyo.

Wacheza shoo wa bendi hiyo wakiwajibika stejini, kukonga nyoyo za mashabiki waliokuwa wamejazana ukumbini humo.

Wacheza shoo wa bendi hiyo wakitia madoido wakati walipokuwa wakiwajibika stejini kwenye onesho hilo.

Wacheza shoo wakionesha ufundi wao wa kuzirudi ngoma za kundi hilo, wakati walipokuwa wajibika stejini.
 
Wacheza shoo wa bendi hiyo, walitia fora sana katika onesho hilo, kwani ilikuwa kama vile waliopagawa kwa kutoa shoo za hali ya juu zilizowaacha mashabiki vinywa wazi. 
 
Hizi ni baadhi tu ya majamboz ya wacheza shoo wa bendi hiyo, jinsi walivyokuwa wakiwajibika jukwaani na kuonesha thamani halisi ya kuwepo kwenye kundi hilo linalopiga muziki wenye asili ya Kizaire. 
 
Sasa angali mwenyewe mambo ya shoo za vijana hao wa kazi wa kundi hilo, zilivyokwenda shule na kumvutia kila mtu aliyesogelea karibu na ukumbi huo katika onesho hilo.

Hii ni moja tu ya staili za shoo zilizokuwa zikipakuliwa na vijana wacheza shoo wa bendi hiyo, ukumbini humo.

No comments:

Post a Comment