TANGAZO


Wednesday, November 7, 2012

Waziri wa Habari wa Zanzibar akutana na waandishi wa Misri

Waziri wa Habari ,Utamaduni, Utalii na Michezo, Said Ali Mbarouk, akizungumza na Ujumbe wa wandishi wa habari kutoka nchini Misri huko Wizarani, mjini Unguja leo. Wandishi hao, walitembelea maeneo kadhaa ya Kiutalii Zanzibar.
Na Ali Issa-Maelezo Zanzibar 07/11/2012
Waziri wa Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo, Said Ali Mbarouk amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzíbar inakusudia kuifanya sekta ya utalii kuongeza nafasi za ajira kwa wananchi wake ili kuinua kipato chao na Taifa kwa ujumla.

Hayo ameyasema leo, huko Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo wakati alipokutana na Waandishi wa Habari kuto nchini Misri waliofika Zanzíbar kujionea shughuli mbalimbali za utalii zinavyofanywa na kuweza kuitangaza Zanzíbar katika nchi ya Misri.

Amesema hali hiyo itafikiwa kwa kuwepo misingi imara ya uwekezaji na kupokea watalii wa daraja la juu ambao wana nafasi kubwa ya kuongeza ajira katika maeneo ya mijini na vijijini ili kuondoa umasikini .

“Unapolikuza soko la utalii nikutangaza utalii hivyo ni matumaini yetu kuona tuna pokea watalii wenye kipato ambao watatoa ajira zaidi katika nchi” alisema Waziri Mbarouk.

Aidha, Waziri huyo alisema kuwa suala hilo litafanikiwa kutokana na kuimarishwa miundo mbinu ya uwekezaji,fukwe zilizo bora, hoteli za kimataifa na mashirikiano mazuri yanayofanywa na wadau wa sekta hiyo ikiwemo mashirika ya ndege ,watembezaji wageni na wawekezaji wa mahoteli.

Alisema hiyo ni nafasi ya kipekee kwani itaongeza nafasi za ajira kwa Wananchi na kupelekea kukua kwa uchumi wa taifa mbapo sekta ya utalii ndio muhimili mkuu wa uchumi kwasasa.

Nae Mkurugenzi Jumuiya ya uwekezaji utalii Zanzíbar (ZATI) Julia Bishop alisema kuwa wanaishukuru sana Serikali ya Mapinduzi ya Zanzíbar kwa kuwapa mashirikiano kikamilifu jambo linalopelekea sekta ya utalii kuimarika bila ya pingamizi.

Julia alisema kwa upande wao wanafanya kazi kubwa kuitangaza Zanzíbar kupitia sekta ya utalii ambapo pia hufaidika pale wageni wanapoingia nchini .

Nae mkuu wa msafara kutoka Ubalozi wa Misri Mwandishi Marwa Taufik alimuelezea Waziri Mbaruok kuridhishwa kwao na mapokezi sambamba na kujua jinsi gani Serikali ya Mapinduzi ilivyojipanga vyema katika kuendeleza sekta ya Utalii nchini.

Tawfik alimuahidi Waziri huyo kuitangaza Zanzíbar kiutalii katika nchi yao ya Misri kutokana na mazingira mazuri ya kiutalii ambayo Zanzíbar imejaaliwa kulinganisha na nchi nyingine.

No comments:

Post a Comment