TANGAZO


Saturday, September 15, 2012

Wanawake Dar es Salaam, wamkaribisha na kupongeza Dk. Asha-Rose Migiro


 Mke wa Rais, Mama Salma Kikwete (katikati), akicheza ngoma ya Segere wakati wa sherehe iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT-CCM), kumkaribisha na kumpongeza, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk. Asha Rose Migiro (kushoto) kwa kuwa mwamamke wa kwanza Afrika kushika wadhifa huo. Hafla hiyo, imefanyika leo viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam. (Picha zote na Richard Mwaikenda)

 Spika wa Bunge, Anne Makinda (kushoto) na Mama Maria Nyerere, wakiangalia wanawake wakiserebuka na muziki wakati wa sherehe hizo.

                           Mama Salma Kikwete, akihutubia katika sherehe hizo.

                       Wanawake wa CCM wakicheza na kufurahi katika sherehe hizo.

 Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Dk. Asha-Rose Migiro (aliyevaa kilemba kushoto), akijumuika kucheza segere wakati wa sherehe, iliyoandaliwa na Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (UWT-CCM), kumkaribisha na kumpongeza kwa kuwa mwamamke wa kwanza Afrika, kushika wadhifa huo, leo kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar es Salaam.

 Mama Migiro akiwapungia wageni mbalimbali na wananchi, mashabiki wa Chama hicho katika sherehe hizo.

Sehemu ya akina mama wakicheza na kufurahi huku wakiwa na mabango ya kumpongeza Dk. Migiro.

No comments:

Post a Comment