TANGAZO


Thursday, September 13, 2012

Mkutano wa 58 wa Mabunge wanachama wa Jumuiya ya Madola (CPA), waendelea Colombo, Srilanka


Mkutano wa 58 wa Umoja wa Mabunge ya Jumiya ya Madola (CPA), umeendelea leo Mjini Colombo, Sri Lanka ambapo Tanzania inashiriki kikamilifu katika kila vikao na washa mbalimbali za Mkutano huo. Katika ufunguzi wa warsha hizo, ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Spika Anne Makinda, unashiriki mijadala hiyo ikiwa ni pamoja na kubadilishana uzoefu wa maswala mbalimbali ya Kibunge na wenzao kutoka Mabunge mengine ya nci za Jumuiya hiyo. 
Pichani juu ni Katibu Mkuu wa CPA, Dk. William Shijja, akihutubia wajumbe wa mkutano wa 58 wa CPA, mjini Colombo Sri Lanka. Pamoja na kutoa maelezo ya awali kuhusu shughuli zote za Mkutano huo wa Mwaka. Dk. Shija ni Katibu Mkuu Mtanzania wa CPA, ambaye anatumikia nafasi hiyo kwa kipindi cha pili sasa tangu 2007.
Spika wa Bunge, Anne Makinda akifuatilia moja wapo ya mada zilizokuwa zikiwasilishwa, wakati wa vikao vya mkutano wa 58 wa CPA, Mjini Colombo Sri Lanka leo. Pembeni yake ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ya Bunge, Mussa Azzan Zungu. Waliokaa Nyuma ni Wabunge Zitto Kabwe na Muhonga Said Ruhwanya.
Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 58 wa CPA, ukifuatilia kwa makini baadhi ya mada zilikuwa zikiwasilishwa katika vikao vya Mkutano huo. Wa Kwanza kushoto ni Mbunge Zitto Kabwe, alieye kulia ni Muhonga Said Ruhwanya na nyuma ya Mbunge Zitto ni Hamad Rashid Muhamed ambao wote, kutoka Tanzania. (Picha zote na mdau wetu)

No comments:

Post a Comment