TANGAZO


Friday, June 22, 2012

Makamu wa Rais Dk. Bilal aiwakilisha Tanzania mkutano wa Mazingira wa UN nchini Brazil

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal, akiwasili kwenye Viwanja vya Ukumbi wa Mikutano, wakati alipofika kuiwakilisha nchi katika Mkutano wa Umoja wa Mataifa (UN), kuhusu Mazingira Endelevu (Rio+20) jana Juni 21, jijini Rio de Janeiro, nchini Brazil. Mkutano huo ni wa pili kufanyika nchini hapa tangu ulipofanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1992. Kushoto kwake ni Balozi wa Tanzania nchini Brazil, Francis Malambugi. (Picha zote na Muhidin Sufiani-OMR)


Makamu wa Rais, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira Endelevu (Rio+20) jana Juni 21, jijini Rio de Janeiro, nchini Brazil jana. 


Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Fatma Fereji, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Terezya Huvisa, wakiwa katika mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira Endelevu (Rio+20) jana Juni 21, jijini Rio de Janeiro, nchini Brazil.

Makamu wa Rais, Dk. Mohammed Gharib Bilal, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Terezya Huvisa (katikati), Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Fatma Fereji na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mahadhi Juma Maalim (kulia nyuma), wakiwa katika Ukumbi wa mkutano, wakati walipohudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira Endelevu (Rio+20) jana Juni 21, jijini Rio de Janeiro, nchini Brazil. 


Balozi Liberata Mulamula (kulia) na Balozi wa Tanzania, nchini Brazil, Francis Malambugi (wa pili mstari wa mbele), wakiwa katika mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira Endelevu (Rio+20) jana Juni 21, jijini Rio de Janeiro, nchini Brazil. Mkutano huo ni wa pili kufanyika nchini hapa tangu ulipofanyika kwa mara ya kwanza mwaka 1992.

Balozi Liberata Mulamula (wa pili kulia), akifurahia jambo baada ya kukutana na Wabunge wa Tanzania. Wa pili kushoto ni Mbunge wa Kahama, James Lembeli, wa pili kushoto ni Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais, Sazi Salula, (katikati) ni Mkurugenzi wa Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais, Dk. Julius Ningu, wakiwa katika Viwanja vya Kumbi za mikutano ya Rio+20, wakati walipofika kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mazingira Endelevu (Rio+20) jijini Rio de Janeiro, nchini Brazil. 

No comments:

Post a Comment