TANGAZO


Monday, May 7, 2012

Rais Shein aanza ziara ya Kusini Unguja

 AfisaTawala wa Mkoa wa Kusini Unguja, Sabri Mohamed, akisoma taarifa ya Mkoa huo, mbele ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein, alipowasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini huko Tunguu, katika ziara ya kutembelea maendeleo ya miradi mbalimbali ya Mkoa huo, katika ziara iliyoanza jleo. (Picha ote na Ramadhan Othman,Ikulu)

 Baadhi ya Mawaziri wa Serikali ya  Mapinduzi ya Zanzibar,walioshiriki katika ziara ya Rais wa Zanzibar  na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed  Shein,wakisikiliza kwa Makini taarifa ya Mkoa wa Kusini Unguja iliyosomwa na Afisa  Tawala wa  Mkoa Sabri Mohamed.

 Viongozi mbalimbali wa Mkoa wa  Kusini, Unguja wakiwa katika mkutano wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, alipoanza  ziara yake mkoani humo  leo na kupata taarifa katika Ofisi ya Mkoa huo, huko Tunguu, Wilaya ya Kati Unguja.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein,(kushoto), akipokea taarifa ya  kazi za utekelezaji wa Mkoa wa Kusini Unguja, kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Mkoa huo, Abdalla Mwinyi Khamis, leo alipoanza ziara yake na  kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo mkoani humo.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Ali Mohamed Shein (kulia), akipata maelezo kutoka  wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamadunu na Michezo, Ali  Mwinyikai, alipotembela eneo jipya linalojengwa Mnara wa Redio wa kurushia  matangazo huko Bungi, Wilaya ya Kati Unguja,alipokuwa katika ziara ya Mkoa  wa Kusini leo.

 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein,(katikati) na ujumbe, aliofuatana nao, wakitoka kuangalia mnara wa Redio ulioanza kufungwa  na  Kampuni ya Ujenzi ya Minara ya New Techinical Contractors Company ya  Dar es Salaam, chini ya Injinia Stivin Makange (mwenye tai), huko Bungi Wilaya  ya Kati Unguja leo, akiwa katika ziara ya Mkoa wa Kusini.

 Rais wa Zanzibar na  Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akisalimiana na Mzanzibari anayeishi nje ya nchi, Dk. Ferouz Jafferji, alipowasili katika Shule ya Sekondari ya Unguja Ukuu, alipotembelea madarasa  ya kusomea  yaliyokarabatiwa na umoja wa Diyasphora pamoja na kuweka jiwe la  msingi wa nyumba ya Madaktari iliyopo jirani na Shule hiyo leo, akiwa  katika  ziara ya Mkoa wa Kusini, Unguja kutembelea  miradi mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa huo.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa  Baraza la Mapinduzi, Dk. Ali Mohamed Shein, akifungua pazia kama ishara  ya uwekaji wa jiwe la msingi wa nyumba ya Madakatari katika kituo cha Afya  cha Unguja Ukuu leo, alipokuwa katika ziara ya kutembelea miradi   mbalimbali ya maendeleo katika Mkoa wa Kusini Unguja, iliyoanza leo, katika Wilaya ya Kati Unguja.

No comments:

Post a Comment