TANGAZO


Thursday, April 12, 2012

Waziri Nundu afungua Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi TCAA, jijini Tanga

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini, Fadhili Manongi, akizungumza katika  ufunguzi wa kwanza wa Baraza la Wafanyakazi  la Mamlaka ya Usafiri wa Anga leo, April 12,2012 jijini Tanga,  wakati alipokuwa akimkaribisha Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu kuufungua mkutano huo. wa  kwanza wa Mkutano wa  kwanza wa Baraza la Wafanyakazi  la Mamlaka ya Usafiri wa Anga April 12, 2012, jijini Tanga. Mkutano huo wa siku mbili, umehudhuriwa na wajumbe 70, wakiwemo, Wakurugenzi Wakuu wa Vitengo, Wakuu wa Vituo, Wajumbe wa Halmashauri ya TUGHE, wajumbe wa kuchaguliwa amabo ni wawakilishi wa wafanyakazi na wajumbe wa kuteuliwa. (Picha zote na Mwanakombo Jumaa- MAELEZO),


Baadhi ya wajumbe hao, wakifuatilia ufunguzi wa mkutano huo, uliofunguliwa na Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu leo.




Wajumbe wakifuatilia hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye ufunguzi huo.






 Wajumbe wa Baraza, wakisikiliza hotuba ya makaribisho iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga nchini, Fadhili Manongi kabla Waziri Nundu kuufungua mkutano huo.




 Wajumbe kwa makini wakimsikiliza mgeni rasmi Waziri wa Uchukuzi hayupo pichani Omari Nundu.




 Wajumbe wakifurahia hotuba iliyokuwa ikitolewa na Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu kwenye ufunguzi wa mkutano wa Baraza hilo jijini Tanga leo. 




Wajumbe wa mkutano wa Baraza la wafanyakazi wakiwa kwenye ukumbi uliokuwa ukifanyika mkutano huo, ukumbi wa Tanga Beach Resort, mjini humo.


 Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu, akiufungua mkutano wa Kwanza wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga mjini Tanga leo, Aprili 12, 2012.




Waziri wa Uchukuzi Omari Nundu (aliesimama), akiufungua Mkutano wa Kwanza  wa Baraza la Wafanyakazi la Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA), leo April 12,2012, jijini Tanga.






 Waziri wa Uchukuzi akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano wa kwanza wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga, mjini humo.




 Wazir wa Uchukuzi,  Omar Nundu (kulia), akipongezwa na  baada ya Ufunguzi wa Baraza na Mkuurugenzi Mkuu wa TCAA Fadhili Manongi, kutokana na hotuba yake, aliyoitoa kwenye ufunguzi huo.




 Waziri wa Uchukuzi, Omari Nundu, akiteta jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Usafiri na Uchukuzi, Saad Fungafunga kwenye mkutano huo.

No comments:

Post a Comment