TANGAZO


Thursday, April 12, 2012

Shuguli za kuaga mwili na mazishi ya Mwakitabu wa CCM, Dodoma

Vijana wa CCM wakibeba jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Ofisa Mwandamizi wa Makao Makuu ya CCM, Gordon Mwakitabu, kuliingiza nyumbani kwa marehemu, eneo la Area C, mjini Dodoma leo, kwa ajili ya kuaga na mazishi yaliyofanyika baadaye kwenye makaburi ya Nkhungu nje kidogo ya mji. Aliyebeba msalaba ni mtoto wa kwanza wa marehemu Mwakitabu, Martin Mwakitabu. (Picha na Bashir Nkoromo)
 Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Wilson Mukama (katikati), akizungumza na Makatibu Wakuu wastaafu wa CCM, Philip Mangula (kushoto) na Yussuf Makamba, wakati wa shughuli za maziko ya aliyekuwa Ofisa Mwandamizi, Makao Makuu ya CCM, Gordon Mwakitabu, mjini Dodoma leo. 


Mjane wa Gordon Mwakitabu, Janeth Mwakitabu, akiangua kilio wakati wa kuuaga mwili wa marehemu mumewe, leo nyumbani kwao, Area C, mjini Dodoma.




Waombolezaji wakiwa nyumbani kwa marehemu Mwakitabu wakati wa kuaga mwili wake.




Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama akiaga mwili wa marehemu Mwakitabu, nyumbani kwa marehemu, Area C, mjini Dodoma leo.




 Makatibu wakuu wastaafu wa CCM, Yussuf Makamba na Philip Mangula wakiuaga mwili wa marehemu Mwakitabu.




Waombolezaji wakiwa katika huzuni na mshangao, wakati wa kuaga mwili wa marehemu Mwakitabu. Waliokaa mbele, kutoka kushoto ni Katibu wa NEC, Mambo ya Nje, Januari Makamba, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara, John Chiligati.





No comments:

Post a Comment