TANGAZO


Monday, April 9, 2012

Tamasha la wanajumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania lafana

Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (kushoto), akizungumza na mgeni rasmi katika tamasha la wanajumuiya hao, Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yussuf Mwenda, wakati wa tamasha hilo, lililofanyika viwanja vya Shule ya Sekondari ya St. Mary's, Sinza Dar es Salaam leo. (Picha zote na Kassim Mbarouk)




Wanajumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, wakicheza moja ya ngoma za Kiganda wakati wa tamasha leo hilo.




 Wasanii Narayenga Annet (kulia), Ritah Nasaka (kushoto) na Hawa Nakalanzi, wakionesha jinsi mwanamke wa Kiganda anavyotakiwa avae, mavazi ya heshima wakati wa kuonesha sanaa ya nyimbo na maigizo kwenye tamasha hilo.




 Wasanii Narayenga Annet (kulia), Ritah Nasaka (kushoto) na Hawa Nakalanzi, wakifurahia mavazi yanayotakiwa kuvaliwa na mwanamke wa Kiganda wakati wa kuonesha sanaa hiyo, kwenye tamasha hilo.



Wanajumuiya hao, wakivutana na kamba katika mchezo wa kuvuta kamba kwa wanaume kwenye tamasha hilo la Uganda family Day, viwanjani hapo.




 Wanajumuiya ya watu wa Uganda waishio Tanzania, wakionesha kukubali kuvutwa na wenzao wa timu pinzani katika mchezo wa kuvuta kamba kwa wanaume.




 Wanajumuiya wa kike wakivutana na kamba katika mchezo wa kuvuta kamba kwa wanawake kwenye tamasha hilo la Uganda family Day, viwanjani hapo.



 Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (kushoto), akizungumza jambo na Afisa Ubalozi wa Uganda nchini Tanzania, Kiyingi Stephen wakati wa  tamasha hilo.




Baadhi ya wanajumiya ya wananchi wa Uganda, waishia Tanzania, wakikimbiza kuku katika mchezo wa kukimbiza kuku wakati wa tamasha hilo.

 Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (kushoto), mgeni rasmi katika tamasha la wanajumuiya hao, Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yussuf Mwenda (katikati) na Makamu Mwenyekiti wa Jumuiya, Hellen Tusiime, wakifuatilia moja ya matukio yaliyokuwa yakitendeka wakati wa tamasha hilo, katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya St. Mary's, Sinza jijini leo. 




 Kijana aliyejitambulisha kwa jina moja tu la Ismail, akiwa na kuku wake aliyemkamata wakati wa mashindano ya kukimbiza kuku kwenye tamasha hilo.




 Baadhi ya wanajumuiya, wakicheza moja ya ngoma za Kiganda zilizokuwa zikipigwa kwenye tamasha hilo.




 Baadhi ya watoto wa wanajumuiya, wakicheza huku wazazi wao wakishiriki kwenye michezo mbalimbali kwenye tamasha lao hilo.



Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (kulia), akicheza na wasanii waliokuwa wakicheza moja ya ngoma za asili ya Waganda, iliyokuwa ikipigwa viwanjani hapo.

 

  Baadhi ya wanajumuiya, wakifurahia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakitendeka kwenye tamasha hilo.


 Msanii Hawa Nakalanzi, akionesha ustadi wake wa kuzicheza ngoma za asili ya Kiganda zilizokuwa zikipigwa kwenye tamasha hilo.






   Baadhi ya wanajumuiya, wakifuatilia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea kwenye tamasha hilo.



  Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (kulia), akicheza na mmoja wa watoto wa wanajumuiya hiyo, huku Makamu wake, Hellen Tusiime (kushoto), akicheza na mwanajumuiya mmoja aliyejitosa kumuunga mkono katika kuzirudi ngoma za Kiganda zilizopigwa kwa ajili ya viongozi hao kulifunga  tamasha hilo.





 Wanajumuiya hawa nao hawakuwa nyuma katika kukumbuka ngoma za nyumbani kwao, hapa wakionesha ufundi wao wa kuzirudi ngoma hizo.




 Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (JB), akizungumza wakati akilifunga tamasha hilo.






Mwenyekiti wa Jumuiya ya wananchi wa Uganda waishio Tanzania, Justus Baguma (JB), akimtambulisha mmoja wa wanajumuiya hiyo, Opherus Musasira, ambaye ameishi nchini Tanzania zaidi ya miaka 20, kwa wanajumuiya hao.


No comments:

Post a Comment