TANGAZO


Saturday, April 7, 2012

Msanii Kanumba hatunaye tena


Msanii Nguli wa Filamu Steven Kanumba Afariki Dunia

Mwigizaji maarufu wa filamu nchini Steven Kanumba amefariki dunia usiku wa kuamkia leo, habari zinasema mwili wa mwigizaji huyo umepelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhibili ili  kufanyiwa uchunguzi na kuhifadhiwa.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi  wa Kinondoni, Charles Kenyela, amethibitisha kutokea kifo cha mwigizaji huyo na kuongeza kwamba sababu za kifo chake bado zinafanyiwa uchunguzi lakini taarifa za mwazo ambazo Polisi wamezipata zinasema Kanumba alikuwa  na mpenzi wake chumbani na kulitokea kutokuelewana kati yao na kusababisha kutokea kwa ugomvi ulipelekea kifo chake.

No comments:

Post a Comment