TANGAZO


Monday, March 26, 2012

Waziri Mkuu Pinda Alipokea Kombe la UEFA jijini Dar

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiwapungua watu waliofika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu, kushuhudia ujio wa kombe la UEFA,  jijini Dar es salaam Machi leo 26, 2012. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa pamoja na Meneja Mkuu wa Bia ya Heinken Afrika Mashariki, Koen Morshiu's wakifunua kitambaa, kuonyesha kombe la Ulaya wakati Kampuni ya bia ya Heinken ambao ndiyo wadhamini wa kombe la Ulaya (UEFA) walipomkabidhi kombe hilo Waziri Mkuu leo, ofisini kwake, Kampuni ya Henken pamoja na Shirikisho la mpira wa miguu la ulaya (UEFA) liko katika ziara ya kulitembeza kombe hilo katika nchi za Afrika na Amerika ya Kusini, Mexico, Asia nchini China,  Tanzania na Kenya.
Waziri Mkuu,  Mizengo Pinda kwa pamoja na Meneja Mkuu wa Bia ya Heinken Afrika Mashariki, KoenMorshiu's wakipiga makofi mara baada ya kufunua kitambaa kuonyesha Kombe la Ulaya UEFA.
Waziri Mkuu Mizengo Pinda akipiga picha na Kombe hilo pamoja na  Waziri wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Emmanuel Mchimbi na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk Fenella Mukangara (kulia) na Makamu wa kwanza wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Athuman Nyamlani.

No comments:

Post a Comment