TANGAZO


Monday, March 19, 2012

Mkuu Mpya wa JKT aapishwa Ikulu jijini Dar es Salaam

  Mkuu Mpya wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Meja Jenerali Samwel Ndomba, akila kiapo mbele ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Meja Jenerali Ndomba anachukua nafasi ya Meja Jenerali Samwel Kitundu, aliyestaafu hivi karibuni kwa mujibu wa sheria. (Picha na Freddy Maro)



  Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akimkabidhi muongozo ya kazi Mkuu mpya wa JKT, Meja Jenerali Samwel Ndomba, wakati wa hafla ya kumuapisha, iliyofanyika leo asubuhi Ikulu jijini Dar es Salaam.



  Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto), Waziri Mkuu Mizengo Pinda (kulia) na Mkuu mpya wa JKT, Meja Jenerali Samwel Ndomba, wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha Mkuu huyo mpya wa JKT, Ikulu jijini Dar es Salaam leo.


  Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Mrisho Kikwete (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Jenerali Davis Mwamunyange (kushoto) na Mkuu mpya wa JKT, Meja Jenerali Samwel Ndomba, muda mfupi baada ya hafla ya kumuapisha iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam leo.



Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akisalimiana na mzee Albert Ndomba (85), baba mzazi wa Mkuu Mpya wa JKT, Meja Jenerali Samwel Ndomba (wapili kushoto), baada ya halfa ya kumuapisha iliyofanyika iIulu jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni mke wa Meja Jenerali Ndomba na waliosimama nyuma ni wanafamilia.




No comments:

Post a Comment