TANGAZO


Tuesday, March 27, 2012

CCM waendelea kuchana chana kwenye kampeni za Ubunge, Arumeru Mashariki

Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi wa Jimbo la Urumeru Mashariki, Sioi Sumari, akiwapungia wananchi wakati alipofika kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Ngarasero, Usa River jana. (Picha na Bashir Nkoromo)
.




Umati wa watu waliofurika mkutano wa kampeni za CCM, Uwanja wa Ngarasero, Usa River, ukinyanyua mikono ili kumuunga mkono mgombea wa Chama hicho, Sioi Sumari.






 Mratibu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba akisoma waraka wa siri unaodaiwa kuandikwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika Usa River jana. Kama ikibainika waraka huo ni wa CHADEMA na wakikiri watashindwa uchaguzi wa Arumeru Mashariki.








Mbunge wa Mtera, Livingstone Lusinde, akihutubia mkutano wa kampeni za CCM kwenye Uwanja huo.



Gari la Polisi likimpeleka kituoni mtu aliyekamatwa kwa  tuhuma za kujaribu kuanzisha fujo kwenye mkutano wa kampeni za CCM, Uwanja wa Ngarasero, Usa River.




Wazee wa Kijiji cha Lekitatu, Usa River wakifuatilia kwa makini mkutanao wa kampeni za CCM, uliofanyika jana kwenye kijiji hicho.






Akina mama wakishangilia mkutano wa kampeni wa mgombea wa Ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sioi Sumari, uliofanyika katika kijiji cha Lekitatu jana.

No comments:

Post a Comment